Mbunge Abwao akiwa na waziri mkuu Mizengo Pinda
Pamoja na kuruhusiwa katika Hospitali ya mkoa wa Iringa ambako mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) Chiku Abwao alikokuwa akitibiwa bado hali yake kiafya ni mbaya .
Mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com umeelezwa kuwa mbunge Abwao kwa sasa amehamishiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam kwa matibabu zaidi baada ya afya yake kuendelea kuteteleka .
Jitihada za kumtafuta mbunge Abwao zinaendelea ili kujua afya yake zaidi kutokana na tatizo hilo la uvimbe katika mguu wake ambalo linamsumbua .
Habari imeandika na Francis Godwin
0 comments:
Post a Comment