Mwandishi wetu, Iringa Yetu
KATIKA hali isiyo ya kawaida,Balozi wa
Marekani nchini ALFONSO LENHARDT amejikuta akishindwa kuamini anachosikia
baada baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Iringa wanaoishi na virusi vya ukimwi
kumshukuru Mungu kwa kuwapatia virusi hivyo.
Wananchi hao walitoa kauli hiyo muda
mfupi baada ya Balozi huyo wa Marekani kuzindua rasmi Kituo cha Afya cha
Alamano kinachoendeshwa na Watawa wa Kanisa Katoliki, kilichokarabatiwa kwa
msaada wa wananchi wa Marekani,kitu ambacho hutoa huduma mbalimbali kwa watu
wanaoishi na virusi vya Ukimwi Manispaa ya Iringa.
Baadhi ya wananchi hao ni Eliza Muhumba
na Bwana Wito Chavala ambao wamedai kuwa huenda Mungu alikuwa na maksudi yake
kuwafanya wapate virusi vya ukimwi kwa maelezo kuwa baada ya kupata virusi
hivyo,maisha yao kiafya na kiuchumi yameimarika zaidi ikilinganishwa na wakati
hawajaambukizwa kutokana na huduma mbalimbali ikiwemo za tiba na mikopo midogo
midogo wanayopata kutoka Alamano Centre
Kufuatia kauli hizo,Balozi wa Marekani
Alfonso Lenhardt alileza kuguswa nazo na kusema kuwa kuimarisha afya za
watanzania ni moja ya vipaumbele vya ubalozi wa Marekani nchini Tanzania
Kwa msaada wa Marekani,Alamano Centre
mpaka sasa inahudumia watu watu wanaoishi na virusi vya ukimwi karibu 4,000
ambapo 2000 wanapata huduma na misaada mbalimbali na 1800 wanapata tiba ya
kupunguza makali ya virusi vya ukimwi.
Blogzamikoa
0 comments:
Post a Comment