Mwandishi wetu, Iringa Yetu
MGOGORO
uliodumu kwa zaidi ya miaka miwili katika Jumuiya ya Matumizi Bora Malihai
Tarafa za Idodi na Pawaga (MBOMIPA) wilaya ya Iringa hatimaye umepatiwa
ufumbuzi na kumalizika.
Vijiji
21 vinavyounda Jumuiya hiyo vilikuwa katika mgogoro mkubwa wa namna ya kugawana
mapato yanayotokana na vyanzo vyake lakini katika Mkutano kati ya Mkuu wa
wilaya ya Iringa,wenyeviti wa vijiji hivyo 21 na Shirika la hifadhi ya
wanyamapori –WCS, mgogoro huo ukapatiwa ufumbuzi.
Vijiji
hivyo 21 ni vijiji vinavypakana na hifadhi ya Taifa ya Ruaha na baadhi yake
vilitoa ardhi kwa ajili ya hifadhi ya jamii na vimekuwa vikipata hadi
Sh.milioni 140 kwa mwaka kutokana na utalii wa picha na uwindaji wa kienyeji na
uwindaji wa kitalii.
Mkuu
huyo wa wilaya Dkt.Reticia Warioba anasema ni wakati sasa wa kusonge mbele kwa
jumuiya hiyo baada ya kumalizika kwa mgogogoro huo.
Awali
Mkurugenzi wa WCS aliwaomba wajumbe wa mkutano hao kujali maslahi ya Jumuiya
kwa kuumaliza mgogoro huo baada ya hali ndani ya ukumbi kuwa tete huku baadhi
ya wenyeviti wa vijiji wakitishia kwenda mahakamani
Kabla
ya mgogoro huo kumalizika, vijiji vinane vilikuwa vimesusa mgawo wa mapato ya
mbomipa vikipinga kugawana sawa ni vijiji ambavyo ama vilitoa ardhi kidogo ya
uhifadhi au havikutoa kabisa.
Blogzamikoa
0 comments:
Post a Comment