Na MatukiodaimaBlog
MBUNGE
wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe amewataka viongozi wa
kisiasa kuweza kujitafakari juu ya nafasi wanazoziongoza ili kuona
kama wapo kwa ajili yao binafsi ama kwa ajili ya jamii
iliyowachagua.
Filikunjombe
alitoa kauli hiyo jana wakati akitoa salam zake za pore kwa
wakazi wa Ludewa katika mazishi ya aliyekuwa mjumbe wa halmashauri
kuu ya Taifa (NEC) wilayani hapo Elizabeth Haule yaliyofanyika
kijijini kwake Luana , kuwa lazima viongozi kujenga utamaduni wa
kuwatumikia wananchi ambao wamewawezesha kuwa na nafasi hizo
badala ya kujinufaisha wao.
Mbunge
Filikunjombe alisema kuwa wilaya ya Ludewa imempoteza kiongozi
imara na kuwa uongozi wa MNEC huyo ulikuwa ni wa kuigwa kutokana
na namna ambavyo alivyokuwa akiwasilisha mambo yake na siku
zote kuonyesha kuwatumikia wana CCM waliomuwezesha kuwa MNEC.
"
Siku mbili kabla ya kifo chake nilipata kuzungumza na marehemu
kupanga juu ya sherehe ya CCM ila alinikumbusha juu ya barabara
ya Malato ,Itundu alikuja kwangu na kuniomba kila wakati .....hadi
siku ya mwisho nikipangana nae mwishoni aliniuliza ahadi yake juu
ya barabara vipi na siku moja nilimtania kuwa wewe ni mkazi wa
Malato na unasali Anglicana na ile barabara inakwenda kanisa la
Roman Katoliki ila alisema wote ni watu wake ....hivyo naomba
nisema siwezi kuacha kutekeleza ombi lake la barabara"
Mbunge
huyo alisema kuwa amepata kujifunza mengi kutoka kwa marehemu
huyo enzi za uhai alikuwa akiomba pasipo kutumia nguvu na moja
kati ya jambo ambalo alikuwa akimuomba ni pamoja na kusaidia
kuchonga barabara ya kijiji hicho kuelekea kanisa la RC lililopo umbali wa zaidi ya Kilometa 5 kutoka barabara kuu ya Ludewa - Njombe .
"
Mimi pia nimepata kujifunza kutoka kwa marehemu huyo kumbe
unaweza kuomba bila kutumia nguvu zaidi na ukapata ....suala hili
la kuniomba kusaidia kuchonga barabara kila wakati amekuwa
akinipigia simu na kuniomba lakini naomba kutamka leo hapa kuwa
nitamuenzi kwa kutengeneza barabara hiyo ambayo hakuna hata
mwananchi mmoja amepata kuniomba barabara hiyo itajengwa mwezi
wa sita na pia nitasogeza umeme kutoka Malato kwenda kitongoji cha
Itundu kuanzia mwezi wa tano mwaka huu"
Alisema
kuwa marehemu alikuwa akiutumia uongozi wake vizuri kwa kuwajali
wananchi wake hivyo ni vema kila kiongozi wa kisiasa kuona
anatumia vema nafasi yake aliyopewa na wananchi kwa kuwatumikia
waliomchagua.
Aidha
alisema kuwa kwa upande wake bungeni akiwa anaomba jambo kwa
ajili ya wana Ludewa siku zote amekuwa akitumia nguvu lakini
marehemu yeye alikuwa akiomba kwa unyenyekevu na siku zote
alikuwa ni mtu wa kuwatumikia wananchi wake hivyo lazima kila
kiongozi wa siasa kujitafakari zaidi .
Marehemu
Haule katika uhai wake mbali ya kuwa mjumbe wa NEC Taifa
akiwakilisha wilaya ya Ludewa pia alikuwa ni mwenyekiti wa UVCCM
wilaya ya Ludewa na mwenyekiti wa kikundi cha Sanaa Ludewa
alifariki kwa ugonjwa wa moyo juzi katika Hospitali ya wilaya ya
Ludewa baada ya kuzidiwa toka jumapili akitokea katika sherehe za
miaka 38 ya kuzaliwa kwa CCM.
|
0 comments:
Post a Comment