MATOKEO
ya awali katika uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Kalenga, Iringa
Vijijini, yanaonesha Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimepata ushindi wa
kishindo katika kata 11 kati ya 13, ambapo idadi ya vituo vya kupigia
kura vilikuwa 200.
Kata hizo ni Lumuri, Kalenga, Kiwere, Mgama,
Ifunda, Magulilwa, Nzihi, Ulanda, Wasa, Lyangungwe na Mseke ambapo kata
za Maboga na Luhota matokeo yake hadi tunakwenda mtamboni yalikuwa
hayajatangazwa.
Kata ya Ifunda inadaiwa kuwa ngome ya chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambacho kilifunga kampeni zake katika
kata hiyo.
Dosari zilizojitokeza katika uchaguzi huo ni pamoja na
baadhi ya wapigakura waliokuwa na shahada za kura, kukuta majina yao
hayapo kwenye vituo vya kupigia kura.
Hata hivyo, mmoja wa
waangalizi wa uchaguzi huo kutoka Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC), aliyefahamika kwa jina la Kaijage, alisema wote ambao
majina yao hayajaonekana lakini wana shahada, wajaze fomu maalumu na
kuruhusiwa kupiga kura.
Matokeo ya awali kwenye vituo, Ofisi ya
Kijiji Tagamenda CCM-64, CHADEMA-53, CHAUSTA-0, Ofisi ya Kijiji
Ugwachana, ccm- 91-CHADEMA-31, CHAUSTA-0,, Ofisi ya Kijiji Tanangozi 1,
CCM- 86, CHADEMA-46, CHAUSTA-2.
Tanangozi 2, CCM-79, CHADEMA-28,
CHAUSTA-0, Shule ya Msingi Mtivila, CCM-83, CHADEMA-17, CHAUSTA-1, Tosa
1, CCM-98, CHADEMA-20- CHAUSTA-0, Ipamba 2, CCM-104, CHADEMA-10,
CHAUSTA-0.
Isakulilo, CCM-83 , CHADEMA-8, CHAUSTA-0, Kilindi A,
CCM-69, CHADEMA-23, CHAUSTA-0, Ofisi ya Kijiji (Kilindi), CCM-117,
CHADEMA-53, CHAUSTA-0, Zahanati CCM 117, CHADEMA-67, CHAUSTA-0.
Kata
ya Ifunda, Kivavali A, CCM-99, CHADEMA-19, CHAUSTA-0, Kivalali B,
CCM-109, CHADEMA-14, CHAUSTA-0, Muwimbi CCM-164, CHADEMA-22, CHAUSTA-0,
Mahanzi CCM-130, CHADEMA-46, CHAUSTA-0.
Ikungwe A, CCM-131,
CHADEMA-23, CHAUSTA-0, Ikungwe B, CCM-216, CHADEMA-13, CHAUSTA-0,
Magunga CCM-184, CHADEMA-4, CHAUSTA-1, Wasa CCM-149, CHADEMA-15,
CHAUSTA-0, Usengelidate CCM-260, CHADEMA-46, CHAUSTA-0.
Kutokana na
matokeo hayo ya awali, wafuasi wa CCM walianza kushangilia ushindi
kwenye maeneo mbalimbali ya jimbo hilo wakiwa wameshika vipande vya miti
na kucheza ngoma.
Utulivu Kalenga
Wakazi wa jimbo hilo,
walijitokeza kwa wingi katika vituo vya kupigia kura ambapo hali ya
amani na utulivu, ilitawala katika maeneo mbalimbali ya jimbo hilo.
Vituo
vya kupigia kura vilifunguliwa saa moja asubuhi ambapo misururu mirefu
ilianza kuonekana muda mfupi baada ya kazi ya kupiga kura kuanza.
Miongoni
mwa vituo vilivyokuwa na idadi kubwa ya wapigakura ni vile vilivyopo
kwenye kata ya Kalenga Mjini, Kata ya Kalenga na Mangalila vilivyo
kwenye Kata ya Ulanda.
Katika Kata ya Maboga, vituo vyote vya
kupigia kura vilifunguliwa mapema ambapo akizungumza na Majira baada ya
kupiga kura, Bw. Onesmo Makasi, mkazi wa Mangalila, alisema awali
alidhani uchaguzi huo utagubikwa na vurugu kutokana na kauli zilizokuwa
zikitolewa na baadhi ya wanasiasa.
"Nimepiga kura kwa amani na utulivu, kutokana na utaratibu huu naamini mshindi atatangazwa mapema," alisema.
Mkazi
mwingine wa kijiji hicho, Zaina Konzi aliipongeza Tume ya Taifa ya
Uchaguzi (NEC) na Jeshi la Polisi kwa kuhakikisha uchaguzi huo unakuwa
wa amani.
Ulinzi uliimarishwa katika vituo vyote vya kupigia kura
ambapo askari mmoja ambaye hakupenda kutaja jina lake kwenye Kituo cha
Kalenga A na B, alisema wamejipanga vizuri kulinda amani na kudhibitio
viashiria vya vurugu.
Helikopta ya Chadema
CHADEMA waliitumia
helkopta yao kuzunguka katika maeneo mbalimbali ya jimbo hilo. Baadhi ya
kata ambazo zilifikiwa na helikopta hiyo ni Kalenga, Nzihi, Ifunda na
Wasa.
Jeshi la Polisi mkoani humo, lilizuia matumizi ya helikopta
siku ya jana ili kuwawezesha wananchi kupiga kura kwa utulivu lakini
CHADEMA waliitumia kwa kutoa nembo ya chama ili kutokiuka sheria na
kanuni za uchaguzi.
Kauli za vitisho
Kabla ya uchaguzi huo,
kauli mbalimbali za vitisho zilikuwa zikitolewa na baadhi ya wanasiasa
walipokuwa kwenye mikutano ya kampeni na kuonekana kuwatia hofu
wananchi.
Kuna zilizodai kuna vijana waliofichwa porini kwa ajili ya
kuzuia watu wasiende kupiga kura hivyo kusababisha hofu kwa baadhi ya
wananchi wakihofia usalama wa maisha yao.
Baadhi ya wananchi
waliamini uchaguzi huo ungegubikwa na vurugu kutokana na kauli za
wanasiasa hao ikiwemo ya baadhi ya makundi ya vijana kuingizwa jimboni
humo.
Kamanda wa Polisi mkoani humo, Ramadhan Mungi alisema polisi
wamejipanga kukabiliana na kila aina ya hila zinazoweza kuvuruga
uchaguzi huo.
Kauli hiyo imesaidia kuimarisha hali ya amani jimboni humo ambapo wapigakura walipiga kura zao bila vitisho.
Vyama
vitatu vilishiriki katika uchaguzi huo ambavyo ni CCM, CHADEMA na
CHAUSTA. Mgombea wa CCM ni Bw. Mgimwa, CHADEMA alikuwa, Bi. Grace
Tendega na CHAUSTA, Bw. Richard Minja.
Hadi tunakwenda mtamboni, NEC ilikuwa haijatangaza rasmi matokeo hayo wala kumtangaza mbunge mteule wa jimbo hilo.
Chanzo:Majira
0 comments:
Post a Comment