Home » » MBUNGE WA JIMBO LA ISMANI WILIAMU LUKUVI APATA WAPINZANI JIMBONI KWAKE

MBUNGE WA JIMBO LA ISMANI WILIAMU LUKUVI APATA WAPINZANI JIMBONI KWAKE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

mtia nia wa ccm jimbo la ismani festo kiswaga akiwa katika ofisi za ccm jimbo la iringa vijiji
akiwa na katibu wa ccm iringa vijijini

NA MWANDISHI WETU,IRINGA.

Baada ya zoezi la uchaguzi wa wagombea urais kukamilika katika vyama sasa zoezi limeanza kwa wabunge na madiwani ambapo hii leo Festo Kiswaga ambaye ameweka nia ya kugombea katika jimbo la isiman.

Katika mkutano huo na waandishi wa habari KIswaga amekanusha uvumi uliokuwa umezagaa juu ya kuhongwa pesa mwaka 2010 ili kutogombea huku akidai kuwa alishindwa kwa haiki na si hongo ya mbunge aliyepo madalakani kwasasa huku akimzawadia ukuu wa wilaya.

Ambapo pia ametumia mkutano huo ili kuujulisha uma juu ya maelengo yake ya kuchukua form katika wasifu wake amesema anadigree ya sayansi ya wanyama poli na kutumikia katika shirika la mbomipa na kuwatumikia wananchi wa misenyi mkoa wa kagera akiwa ni mkuu wa wilaya na sasa ni mkuu wa wilaya ya Nanyumbu huku akitumikia mashirika kama tanapa na chuo kikuu cha dar es-laam na kuteuliwa kuwa rais wa wa shirikisho vyuo vikuu vya umoja wa Afrika mashariki uliojumuisha vyou vikuu zaidi ya  400 katika nchi za Tanzania,Uganda,Kenya na Burundi.

Akizungumzia kuhusu janga la njaa lililopo katika jimbo hilo amekiri kuwa anauzoefu juu ya utatuzi wa matatizo kama hayo kutokana na nyanja mbalimbali ambazo amepitia na pia amewataka wananchi wa ismani kumpa lidhaa yya kuwaongoza kutokana tatizo kama hilo amelikuta katika wilaya ya Namnyumbu na akafanikiwa kulitatua kwa asilimia 100%.

Aidha amesema kutokana na jimbo hilo kukosa kiongozi mwenye uchungu kama yeye imepelekea kukosekana kwa huduma kama maji katika vijiji mbalimbali ikiwa jimbo hilo limefikisha miaka 20 ikiwa mashirika mbalimbali na serikali licha ya kuchangia lakini ukosefu wa maji umekuwa tatizo si kwa binadamu tuu bali hata kwa mifugo ambapo hupelekea wananchi kununua maji hadi kwa shiringi mia 500.

Kwaupande wa wananchi waliohudhulia mkutano huo wamekiri kuwapo kwa tatizo hilo ambalo imekuwapo kwa miaka mingi sasa hali inyopelekea wananchi upeleka mifugo yao kunywesha usiku wa manane hali ambayo ineza kuhatarisha usalama wa mifugo hiyo.



Nao kinamama wamekiri kuwa tatizo hilo limekuwa likiwaathiri kiuchumi kwakuwa hutumia muda mwingi katika kutafuta maji bila kufanya shughuli nyingine kwaajiri ya kujenga uchumi wao na wanchi.


0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa