Home » » KAMPUNI ZA ASAS ZAONGOZA KWA ULIPAJI KODI BORA KWA MKOA WA IRINGA‏

KAMPUNI ZA ASAS ZAONGOZA KWA ULIPAJI KODI BORA KWA MKOA WA IRINGA‏

Mkurugenzi  wa makampuni ya  Asas  Bw  Salim Abri  Asas  kushoto akipokea cheti  maalum kutoka kwa kaimu mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Letici Warioba  baada ya  kuibuka  mshindi wa kwanza katika  ulipaji kodi mkoa wa Iringa leo
Meneja  wa TRA mkoa wa Iringa Rosalia Mwenda akimpongeza  Bw  Asas  kwa ushindi katika ulipaji kodi
Cheti  kilichotolewa kwa  kampuni ya Asas
Salim Asas  akionyesha  cheti kwa wanahabari  baada ya  kukabidhiwa  cheti  hicho kwa kuwa mlipaji  kodi mzuri
Salim Asas akionyesha  cheti  cha ulipaji kodi bora 
Mzee Kaundama  akipokea  cheti
Meneja  wa TRA  Iringa Bi Mwenda akitoa maelezo ya  awali
Meza  kuu
Mfanyabiashara  Kaundama akijitambulisha
Wanafunzi  wakiigiza  igizo la matumizi ya mashine ya EFDS
Wadau wa TRA  Iringa  wakiwa katika sherehe ya siku ya mlipa kodi
Baadhi ya  waalikwa wakishuhudia
Msanii Iringa akionyesha ujuzi wa kucheza na nyoka aina ya chatu
Wanafunzi wakihamasisha  ulipaji kodi
Watumishi wa TRA  Iringa  wakijadili jambo kabla ya  sherehe hiyo kuanza
Mgeni  rasmi katika  siku ya mlipa kodi mkoa wa Iringa Dr  Leticia  warioba kulia akimkabidhi cheti  mfanyabiashara  Salim Asas   kutoka makampuni ya usafirishaji  mizigo   la Asas Transporters Co. Ltd    na  ile ya   usafilishaji wa mafuta ya  TransFuel Logistics Ltd  baada ya  kuongoza  kwa  ulipaji mzuri  wa  kodi kwa mwaka 2013 /2014
Mgeni  rasmi katika  siku ya mlipa kodi mkoa wa Iringa Dr  Leticia  warioba kulia akimkabidhi cheti  mfanyabiashara  Salim Asas   kutoka makampuni ya usafirishaji  mizigo   la Asas Transporters Co. Ltd    na  ile ya   usafilishaji wa mafuta ya  TransFuel Logistics Ltd  baada ya  kuongoza  kwa  ulipaji mzuri  wa  kodi kwa mwaka 2013 /2014.
Mlipaji kodi mdogo Iringa Shakra  kiwanga akippongezwa kwa  ushindi wa  pili
Salim Asas  akihojiwa na  wanahabari  mkoani Iringa kuhusu  tuzo  mbili alkizopata kwa kuongoza katika ulipaji wa kodi mkoa wa Iringa
Waandishi  wa habari Iringa  wakimhoji Salim Asas  baada ya  kutangazwa mshindi wa kwanza kwa  ulipaji mzuri wa kodi mkoa wa Iringa
Na matukiodaimaBlogu.
WAKATI maadhimisho ya  siku ya mlipakodi nchini yameadhimisha leo nchini kote mamlaka ya mapato  Tanzania (TRA) mkoa  wa Iringa  imekabidhi  tuzo  mbili kwa a makampuni mawili  yanayomilikiwa na familia ya kamanda wa UV CCM mkoa  wa Iringa Bw Salim Asas likiwemo kampuni la  usafirishaji  mizigo   la Asas Transporters Co. Ltd    na  ile ya   usafilishaji wa mafuta ya  TransFuel Logistics Ltd  baada ya  kuongoza  kwa  ulipaji mzuri  wa  kodi kwa mwaka 2013 /2014.


Akitangaza  washindi hao   wakati  wa maadhimisho ya  siku ya mlipa kodi yaliyofanyika  kimkoa katika ukumbi wa IDYDC  mjini Iringa meneja  wa  mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) mkoa  wa Iringa Rosalia Mwenda alisema  kuwa    TRA  imekuwa na utaratibu  wa  kuadhimisha  siku ya mlipa kodi nchini na kuwa kwa  mkoa wa Iringa na  Njombe maadhimisho hayo yamefanyika katika mkoa  wa Iringa  kutokana na mamlaka  hiyo  kuendelea kufanya kazi kama mkoa mmoja .

Alisema  kuwa kampuni  hizo  za  Asas  zimeweza  kuongoza katika  ulipaji kodi katika kipengele  cha mfanyabiashara mlipaji kodi mkubwa baada ya  makampuni mawili  yanayosimamiwa na Asas moja kushika nafasi ya kwanza ambalo ni  lile  kampuni ya  usafirishaji ya Asas Transporters  C. Ltd    kwa  ulipaji kodi  na nafasi ya  pili ya walipaji kodi wa kati  pia imechukuliwa na  kampuni ya usafirishaji  mafuta ya Transfuel Logistics Ltd ambayo  pia  ni  sehemu ya makampuni ya shiriki ya Asas

Aliwataja  wengine   walioongoza katika  ulipaji kodi  kuwa ni pamoja na MT Huel Transporters , ambayo  ilishika nafasi ya  pili na nafasi ya tatu  kwa  walipaji  kodi wakubwa ni  pamoja na Ruaha  University  College   huku  upande  wa  walipaji  kodi  wa kati  aliyeongoza na Iringa Foods and  Deverages Ltd  nafasi ya  pili Transfuel Logistics Ltd na nafasi ya tatu  Kalenga West Parki Tours MOtel Ltd .

Wakati kwa  wafanyabiashara  wadogo  walioshinda  tuzo  hizo  za  vyeti  maalum  nafasi ya  ya kwanza  alipewa BEder F. Kileo nafasi ya  pili  ilichukuliwa na Shakra  Kiwanga  ambae ni mwenyekiti  wa UWT  wilaya ya  Iringa na nafasi ya  tatu  ilichukuliwa na Ahmed Tasha wakati  kwa  mshindi  wa  jumla  kwa mkoa wa Iringa na kanda ya nyanda  za  juu  kusini akipewa  tuzo hiyo Sao Hill Forest Project .

Kwa  upande  wa  vituo vya  radio   kampuni ya  Big  Time  Hinghland  co.Ltd(Radio  Ebony Fm) nafasi ya  pili kampuni ya  Scope Tanzania Ltd ( Radio Countyr  Fm) na nafasi  ya  tatu Qiblatain  Fm  Radio .

Wakati  kwa upande  wa  walipakodi  bora  wilayani  kwa    Mufindi ni SAo Hill Forest Project  iliyoshika nafasi ya  kwanza na ya pili na ya tatu  kuchukuliwa na Chai Bora Ltd  wakati  wilaya ya Ludewa  ni John  Naoel Haule   ,nafasi ya pili  ni Donata Linus MGaya  huku nafasi ya tatu   ni Nathanael Mgaya ,  katika  wilaya ya  Makete  aliyeongoza ni Felix Eliud Sanga , Christopher s.   Mahenge  na  nafasi ya Tatu ni Shaibustolen  Mahenge .

Wilaya ya  Njombe  mshindi  wa kwanza ni  Philemon N . Mtewele   nafasi ya  pili ni Augustino L . Kisinga  na nafasi ya tatu kwa  ulipaji kodi ni  Ndimi Enterprises Ltd .

Akizungumza  baada ya  kukabidhiwa   tuzo  hiyo  mkurugenzi  wa kampuni  za  Asas  Bw  Salim Abri asas  ambae ni kamanda wa UV CCM mkoa  wa Iringa  alisem a kuwa  wajibu  wa kampuni yake ni  kuendelea  kulipa kodi vizuri kama  sehemu ya  kukuza uchumi wa Taifa na  kuwa  tuzo hizo ni  heshima kwa kampuni  zake na kuwa  ni chachu kwa  wengine  kupenda  kulipa kodi .

Pia  alisema  wapo ambao wanafikra  tofauti  kuwa  ukiwa mwanasiasa  ni mtu  wa  kukwepa  kodi na  kuwa kampuni  zake  zipo kwa ajili ya  kuona  uchumi wa Taifa  unakua  pamoja na kulipa  kodi kwa  wakati na  kwa mujibu  wa taratibu za  nchi .

Hata  hivyo  alisema kuwa ukwepaji  kodi  hausaidii hata  kidogo kwa ukuzaji wa uchumi wa Taifa na  kuwa kila mfanyabiashara  anapaswa  kuwa mzalendo na Taifa  lake kwa  kulipa  kodi badala ya  kukwepa  kulipa  kodi .

" Na mimi napenda  kushukuru  sana TRA kwa utaratibu  huu wa  kuwatambua walipaji kodi wazuri na kuwapa vyeti hii ni heshima  na changamoto  kubwa kwa wafanyabiashara  wengine  kulipa  kodi vizuri "

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa