KAULI YA KWANZA YA ABDUL NONDO BAADA YA KUACHIWA KWA DHAMANA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) Abdul Nondo kwa mra ya kwanza amefunguka na kuwashukuru watanzania baada ya kuachiwa kwa dhamana katika mahakama ya Hakimu Mkazi, Mkoa wa Iringa leo Machi 26, 2018

Nondo ameweka wazi hayo baada ya kuachiwa huru na kusema kuwa sasa anaweza kuendelea na masomo yake pamoja na kesi hiyo ambayo itakuwa ikiendelea mkoani Iringa.

"Namshukuru sana wakili Jebra Kombole na wakili wangu mwingine wa Iringa mbali na hapo napenda kuwashukuru wadhamini wangu kwa sababu masharti ya dhamana yalikuwa yanahitaji wadhamini kutoka mkoa wa Iringa kwa hiyo nimepata wadhamini mkoa wa Iringa Mungu awabariki sana.

"Saizi nipo huru naweza kwenda kuendelea na chuo huku nikiendelea na kesi mkoa wa Iringa. 

"Pia nawashukuru Afisa Magereza kwenye eneo ambalo nilikuwa nikiishi katika kusubiria dhamana wamenitunza vizuri kwa upendo na ushirikiano mkubwa hivyo nawashukuru wazazi wangu na Watanzania Mungu awabariki sina zaidi ya zaidi ya hayo" alisema Nondo

Kesi ya Abdul Nondo itatajwa tena tarehe 10 mwezi wa nne mwaka huu mkoani Iringa ambapo wataanza kusikiliza hoja za awali, wakili wa Nondo amewataka watanzani kuwa na subira juu ya jambo hilo kwa kuwa tayari lipo mahakamani hivyo litafahamika.

Waziri Mwakyembe atembelea Maeneo yaliyotumika harakati za Ukombozi na ya kihistoria Mkoani Iringa

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akisalimiana na Chief wa kihehe Evaristo Sambiligunga Mwambeta alipokutana na machief wa kihehe kuzungumza nao kuhusu namna ya kuhifadhi historia ya ukomboziwa Bara la Afrika kwa vizazi vijavyo jana Mkoani Iringa
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akizungumza na Machief wa kihehe (hawapo pichani) alipokutana nao kuzungumzia namna ya kuhifadhi historia ya ukombozi wa Bara la Afrika kwa vizazi vijavyo jana Mkoani Iringa
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (wapili kulia) katika picha ya pamoja na machief wa kihehe baada ya kuzungumza nao kuhusu namna ya kuhifadhi historia ya ukomboziwa Bara la Afrika kwa vizazi vijavyo jana Mkoani Iringa
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (watatu kushoto) akiwasili katika makumbusho ya Mtwa Mkwawa yaliyopo Kalenga kwa ajili ya kuona naoma makumbusho hiyo inavyohifadhi na kuendeleza historia ya shujaa Mkwawa aliyepigana vita vya msituni wakati wa harakati za kuwakomboa wahehe kutoka kwa utumwa wa wajerumani jana Mkoani Iringa. Watatu kulia ni Mratibu wa Programu ya Urithi wa Ukombozi wa Bara la Afrika Bibi. Ingiahedi Mduma
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (wapili kushoto) akiangalia fuvu la Mtwa Mkwawa alipotembelea makumbusho ya Mkwawa yaliyopo Kalenga kwa ajili ya kuona naoma makumbusho hiyo inavyohifadhi na kuendeleza historia ya shujaa Mkwawa aliyepigana vita vya msituni wakati wa harakati za kuwakomboa wahehe kutoka kwa utumwa wa wajerumani jana Mkoani Iringa.
Mtaalamu kutoka makumbusho Mkwawa (kulia) akimuonyesha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Harrion Mwakyembe (wapili kulia) baadhi ya vifaa alivyotumia Mtwa Mkwawa wakati wa harakati za kuwakomboa wahehe kutoka katika utumwa wa wajerumani jana katika makumbusho ya Mkwawa iliyopo katika Halmashauri ya Iringa Mkoa wa Iringa.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akiwa ameshika silaha za jadi alizokuwa anatumia Mtwa Mkwawa wakati wa harakati za kuwakomboa wahehe kutoka katika utumwa wa wajerumani jana katika makumbusho ya Mkwawa iliyopo katika Halmashauri ya Iringa Mkoa wa Iringa.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akiangalia kaburi la Mtwa Abdul Adam Sapi Mkwawa alipotembelea makaburi ya machief kutoka ukoo wa Mkwawa jana katika makumbusho ya Mkwawa iliyopo katika Halmashauri ya Iringa Mkoa wa Iringa.
Mwanafunzi kutoka Shule ya Msingi Muungano akijibu swali la kihistoria lililoulizwa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe wakati wa ziara yake katika mnara wa Frelimo ulipo katika shule ya Muungano jana Mkoani Iringa
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Msingi Muungano iliyopo katika mnara wa Frelimo alipotembelea mnara wa Frelimo uliojengea na serikali ya Tanzania mwaka 1977 kwa lengo la kutoa heshima na kumbukumbu kwa aliyekuwa kiongozi wa chama cha ukombozi nchini Mozambiki Bw. Samora Machel.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (watatu kushoto) katika picha ya pamoja na viongozi kutoka Halmashauri ya Iringa katika mnara wa Frelimo uliojengea na serikali ya Tanzania mwaka 1977 kwa lengo la kutoa heshima na kumbukumbu kwa aliyekuwa kiongozi wa chama cha ukombozi nchini Mozambiki Bw. Samora Machel.

Mhadhiri kutoka chuo kikuu cha Tumaini Dkt. Gibson Sanga (kushoto) akimuonyesha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) baadhi ya vifaa vya kitamaduni vinavyotumiwa na kabila la wahehe alipotembelea makumbusho ya Iringa jana Mkoani Iringa.Picha na: Genofeva Matemu – WHUSM

HALMASHAURI YA MJI MAFINGA YAPITISHA RASIMU YA BAJETI YA MAENDELEO KIASI CHA SHILINGI BILIONI 25.9 KWA MWAKA WA FEDHA 2018-2019

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 





Halmashauri ya mji wa Mafinga imepitisha rasimu hiyo ya bajeti ya maendeleo katika  kikao cha baraza la waheshimiwa madiwani kilichofanyika 26/2/2018 katika ukumbi wa halmashauli ambapo jumla ya fedha kiasi cha shilingi bilioni 25.9 zilipitishwa. 
Akiwasilisha rasimu hiyo ya bajeti kwa wajumbe wa kikao hicho kwa niaba ya mkurugenzi  Afisa mipango wa halmashauri ndugu Andambike kyomo amesema halmashauri ya mji wa mafinga imejipanga katika kuboresha namna ya utoaji wa huduma bora kwa wananchi kwa kujikita katika vipaumbele vitano vya halmashauri ambavyo ni kuboresha makusanyo mapato ya ndani ili kujenga stendi ya kisasa eneo la kinyanambo na kuboresha mazingira ya uwekezaji na ujenzi wa viwanda,pili ni kuboreshakwa kutenga fedha ili kugharamia uendeshaji ujenzi na ukarabati wa vituo vya kutolea huduma za afya na elimu.

Afisa mipango ndugu Kyomo  alindelea kuwasilisha kipaumbele cha tatu kuwa ni kuboresha utendaji kazi wa watumishi wa umma kwa kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kufanyia kazi,ujenzi wa nyumba za watumishi na kutenga fedha za mishahara kwa kuzingatia ikama wakati kipaumbele cha nne ni kuboresha uratibu, usimamizi na utekelezaji wa shughuli mbalimbali  zinazotolewa na halmashauri kwa wananchi kwa kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya ununuzi wa magari matatu (3) ya kuimarisha usimamizi na ufuatiaji huku kipaumbele cha tano ikiwa ni kuimarisha utawala bora kwa kufanya vikao vya kisheria vya halmashauri na kuimarisha mifumo ya  utendaji.

Lengo kuu la bajeti ni kutekeleza malengo ya dira ya Taifa ya maendeleleo 2025 na malengo ya milenia na mpango wa maendeleo endelevu (SDG’s) ambapo kwa pamoja yanaelekeza kupunguza umasikini iliokithiri na njaa,elimu ya msingi kwa wote,usawa wa kijinsia,kupunguza vifo vya watoto, kupunguza vifovya uzazi, utunzaji wa mazingira,kukabiliana na janga la UKIMWI na kujenga uchumi imara wenye kuhimili ushindani.

Mambo mengine muhimu yaliyozingatiwa katika uandaaji wa bajeti  ni pamoja na Hotuba ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dk. John Pombe Joseph Magufuli wakati akifungua rasmi Bunge jipya la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania,Dodoma tarehe 20 Novemba 2015 ambayo pamoja na mambo mengine inaelekeza kupunguza kero na kusogeza huduma kwa wananchi.
 

KASESELA, ASIA JUMA WATINGA KARIAKOO DAR ES SALAAM, LEO, KUPATA UZOEFU WA NAMNA BORA YA KUSIMAMIA VEMA MACHINGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera akisalimia wananchi baada ya kutambulishwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema (watatu kushoto) alipowapeleka Kasesera na Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Juma Abdallah katika eneo la biashara za Machinga katika Mtaa wa Kongo, Kariakoo jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kupata uzoefu wa namna Wilaya ya Ilala ilivyofanikiwa katika kuboresha mazingira na kuwaweka pamoja machinga hao katika shughuli zao. Wapili kushoto ni Katibu Tawala wa Ilala Edward Mpogolo.
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akimtambulisha Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Juma Abdallah kwa Machinga wakati wa ziara hiyo
 Baadhi ya kinamama wakimweleza kero Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema alipokuwa na ugeni huo
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera akiwa katika Mtaa wa Kongo kujionea shughuli mbalimbali zinavyoendesha na Machinga wa Kariakoo
 Msafara wa Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera ukipita katika mitaa mbalimbali ya Kariakoo kujionea shughuli mbalimbali zinavyoendesha na Machinga
 Kasesera akiwa na Mwenyekiti wa Machinga wa kariakoo katika ziara hiyo
 Mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesera akitazama bidhaa za machinga ambazo alisema hadhi ya bidhaa hizo inaonekana ni zaidi na za machinga
 Kasesera akitazama sampuli ya baadhi ya vifaa vya jikoni vinavyofanya kazi ambavyo anauza Machinga
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ricard Kasesera akihoji mfumo kwenye kompyuta alipoingia katika Ofisi ya Umoja wa Machinga kujua wanavyofanya kazi.
 Machinga ambaye ni mtaalamu wa programu za kompyuta namoyo Yusuf, akimpa maelezo Kasesera ya namna ambavyo Umoja wa Machinga unavyohifadhi kumbukumbu zote za machinga katika komyupta. Kulia ni Mbunge wa Kilolo Asia Juma akifuatilia kwa karibu
 Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Asia Juma akimweleza jambo Ofisa katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya walipokuwa kwenye ofisi hiyo ya Machinga Kariakoo
 Kasesera na ujumbe wake wakitoka katika Ofisi ya Machinga
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera na Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Juma wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Machinga wakati wa ziara hiyo
 Kasesera akimfurahia Ustadhi ambaye ni mmoja wa machinga Kariakoo
 Kasesera akifurahia jezi la Timu ya Machinga baada ya kuzawadiwa katika ziara hiyo 
 Kasesera na Amina wakichagua nguo kwenye vitalu vya biashara za Machinga wakati wa ziara hiyo
 Kasesera akilipa fedha baada ya kuchagua nguo alizopenda
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera akiagana na Mwenyekiti wa Machinga Stephen Lusinde mwishoni mwa ziara hiyo 
 Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesera akifanya majumuisho na ujumbe wake bada ya kurudi katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo akifanya utambulisho na kutoa maelezo machache kabla ya kuanza ziara hiyo
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akizungumza ofisini kwake na ujumbe huo kabla ya ziara hiyo kuanza
 Kasesera akizungumza katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala kabla ya ziara kuanza
Kasesera na ujumbe wake wakijiandaa kuondoka ofisi kwa Mkuu wa wilaya kuanza ziara hiyo. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO -

CCM MKOA WA IRINGA UMETOA MSAADA WA BATI 300 NA MIFUKO YA SARUJI 500 KWA HALMASHAURI YA MANISPAA YA IRINGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Katibu wa chama cha mapinduzi Mkoa wa Iringa Christopher Magala akizungumzia utekelezaji wa ila ya chama cha mapinduzi Mkoa wa Iringa
 Na hii ni baadhi ya mifuko ya saruji na bati walizopewa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa

 Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi manispaa ya Iringa Said Rubeya akifanya kazi kwa vitendo wakati wa hafla ya kukabidhi msaada huo 
 Mwenyekiti wa umoja wa vijana Mkoa wa Iringa Kenani kihongosi akifanya kazi kwa vitendo
 Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Iringa Ritta Kabati akifanya kazi kwa vitendo 



Na Fredy Mgunda, Iringa.

Chama cha mapinduzi mkoa wa Iringa kimeanzimisha miaka arobain na moja (41) kwa kutoa msaada wa bati mia tatu (300) na mifuko ya saruji mia tano (500) kwa halmashauri ya Manispaa ya Iringa kwa ajili ya kusaidia ukarabati na ujenzi kwenye shule zenye mahitaji hayo kwa kufanya kazi za kimaendeleo 
 
Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo Katibu wa chama cha mapinduzi Mkoa wa Iringa Christopher Magala alisema kuwa wameamua kutoa msaada kwa kutimiza malengo ya ilani ya chama cha mapinduzi  ya mwaka 2015 hadi 2020 kwa kuwatumikia wananchi waliowaweka madarakani hivyo kufanya ni sehemu ya kazi za chama.

“Tunachokifanya hii leo ni kuendelea kuonyesha wananchi waliotuweka madarakani jinsi gani tunavyofanya kazi kwa mjibu wa ilani yetu kama mwenyekiti wa chama Dr John Pombe Magufuli anavyotekeleza vizuri ilani yetu” alisema Magala

Magala alisema kuwa halmashauri ya manispaa ya Iringa imekuwa kama yatima kimaendeleo kutokana na utendaji kazi wa viongozi wanayoingoza halmashauri hivyo chama cha mapinduzi mkoa wa Iringa kimeamua kuanza kufanya kazi za kimaendeleo kwa wananchi.

“Leo hii hakuna kitu kipya ambacho kimefanya na halmashauri ya Iringa ndio maana tumeingia kazini kufanya kazi kwa nguvu zetu zote hivyo tutawatumikia wananchi ipasavyo na kuhakikisha manispaa inasonga mbele kimaendeleo” alisema Magala

Magala alisema kuwa wameamua kukabidhi misaada hiyo sambamba na kufanya kazi katika shule ya sekondari ya Mawelewele iliyopo kata ya Mwangata kama mfano wa kuikwa kwa wananchi wa kata hiyo sambamba na wanafunzi na viongozi wengine kufanya kazi kwa vitendo na sio kukaa tu maofisini.

“Leo tunakabidhi kama mfano tu wa msaada wetu hapa shuleni tunatoa bati mia hamsini na mifuko ya saruji sitini kwa lengo la kusaidia kumalizika kwa ujenzi huu ambao unaendelea hii leo hivyo naomba uupokee msaada huu ambao najua kwa kiasi furani utachangia maendeleo ya shule hii” alisema Magala

Aidha Magala aliwataka walimu wa shule hiyo kufundisha kwa kuhudi na maarifa ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi wa shule hiyo kwa kuwa serikali inatoa elimu bure bila malipo na kufanikisha kila mtoa apate elimu inayostali.

“Naombeni na sitaki kusikia kuna mtoto amefukuzwa shule kwa kukosa ada wala michango yoyote ile hapo mtanijua mimi nani na jinsi gani navyosimamia ilani ya chama changu hivyo naomba mfanye majukumu yenu kama mnavyotakiwa kufanya” alisema Magala

Magala aliwataka viongozi wote wa mkoa,wilaya, kata hadi tawi kuhakikisha wanafanya kazi vuizuri kwa kusimamia ilani ya chama cha mapinduzi ili kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi ambao wamewaka madarakani.

Baada ya kupokea msaada huo mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela alikishukuru chama cham mapinduzi mkoa wa Iringa kwa kutoa msaada huo ambazo utasaidia kutatua matatizo ya miundimbinu ya shule za manispaa ya Iringa ambazo zipo taabani kabisa.

“Kazi mnayoifanya kweli ilitakiwa kufanywa na serikali ya halmashauri ya manispaa ya Iringa lakini imeshindwa hivyo naomba nitoe shukrani zangu za dhati kwa viongozi wangu wote CCM mkoa wa Iringa kwa kazi kubwa mnayoifanya kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo” alisema Kasesela

Kasesela aliongeza kuwa kuwepo kwa upinzani ndani ya halmashuri ya manispaa ya Iringa kunarudisha nyuma maendeleo ya wananchi kwa kuwa wapinzani hawafanyika kazi kama inavyostahili hivyo tunaomba viongozi wa chama mtusaidie msaada wa kutuletea maendeleo.

“Halmashauri ya manispaa ya Iringa ni yatima hivyo tunaomba chama cha mapinduzi kupitia viongozi wangu mtusaidie kufanya shughuli za kimaendeleo msiishie leo tu maanakuna vitu vingi bado havijakaa sawa” alisema Kasesela

Kasesela akatoa agizo kwa kiongozi yeyoto Yule atakayetumia vibaya msaada huo ulitolewa na chama cha mapinduzi atakula naye sahani moja hadi atajuta kwa kwanini ametumia vibaya msaada huo.
 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa