Zaidi
ya wanafunzi 5,100 wa shule za msingi Wilayani Mufindi Mkoani Iringa,
wanatarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza baada ya kufaulu mtihani
wa darasa la 07 ulifanyika mapema mwaka jana, huku ufaulu huo ukipanda
na kufikia asilimia 80.39 ukilinganisha na asilimia 68.21 ya mwaka 2014.
Taarifa
ya kitengo cha habari na mawasiliano cha halmashauri ya wilaya ya
mufindi kwa nyombo vya habari, imetanabaisha kuwa, wanafunzi waliokuwa
wamesajiliwa kufanya mtihani walikuwa 7,220 na miongoni mwao
waliofaulu na kuchaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari ni 5,198.
Taarifa
hiyo imeainisha mgawavyo wa wanafunzi hao kwa kuzingatia jinsi, ambapo
kati ya waliofaulu, wasichana wameongoza kwa takwimu za ufaulu huo
wakiwa elfu 2,831 wakifuatiwa na wavulana 2,367. Aidha, wanafunzi wote
waliofaulu wamepangiwa shule ili kuendelea na elimu ya sekondari
itakayokuwa ikitolewa bure hapa nchini.
Wilaya ya Mufindi yenye jumla ya shule za msingi 178 imeshika nafasi ya pili Mkoani Iringa kwa kufaulisha wanafunzi wengi kwaasilimia 80.39 ikitanguliwa na Manispaa ya Iringa iliyofaulisha kwaasilimia 80.55 ikiwa na jumla ya shule za msingi 50.
0 comments:
Post a Comment