Kiswaga akimkabidhi kompyuta mkuu wa shule ya Kaning’ombe Bw Mohamed Mchamba (kushoto) |
Viongozi wakifurahia msaada huo |
Mdau wa maendeleo katika jimbo la Kalenga mkoani Iringa Jackson
Kiswaga ambae ni mkazi wa kijiji cha Nyamihuu amezidi kusaidia
maendeleo ya wakazi wa jimbo la Kalenga kwa kukabidhi msaada wa
kompyuta na printa katika shule ya msingi Kaning’ombe .
Msaada
huo umetolewa jana na Kiswaga kama utekelezaji wa maombi ya wazazi
na uongozi wa shule hiyo ambao mwaka jana wakati wa mahafali
walimwombe kuwasaidia vifaa hivyo ili kusaidia kuchapa na kuprinti
mitihani ya wanafunzi shuleni hapo.
Akizungumza
mara baada ya kukabidhi msaada huo Kiswaga alisema kuwa furaha
yake kuona wanafunzi shuleni hapo wanajifunza komyupta na uongozi
wa shule hiyo unapata kitendea kazi kwa ajili ya kufanyia kazi za
wanafunzi.
Kwani
alisema kuwa kompyuta hiyo itawasaidia kuchapa mitihani ya
wanafunzi na kuondoa kero kubwa ambayo walikuwa wakiipata awali kwa
kusafiri zaidi ya km 30 kwenda mjini Iringa kuchapa mitihani ya
wanafunzi.
Hata
hivyo Kiswaga alisema kwa kuwa eneo hilo hakuna umeme na kifaa
hicho kinahitaji umeme atawasaidia msaada wa genereta kwa ajili ya
kusaidia umeme katika utumiaji wa kompyuta hiyo.
Pia alisema akiwa kama mdau wa maendeleo katika
jimbo hilo ataakikisha aaendelea kusaidia pale ambapo atakuwa na
uwezo napo huku kuhusu maombi ya wananchi hao kufikishiwa huduma ya
mtandao wa simu kwa kufungiwa mnala wa tigo alisema kuwa mambi hayo
atayafikisha kwa viongozi wake wa juu ili kuangalia uwezekano wa kusaidia japo alisema hawezi wadanganya kuwa atafikisha mnala huo kesho .
Mkuu wa shule hiyo Mohamed Mchamba mbali ya kumshukuru Kiswaga kwa msaada huo bado alisema kuwa jitihada kubwa zinazofanywa na mdau huyo ni ukombozi katika sekta ya elimu shuleni hapo.
Kwani
alisema kuwa shule hiyo toka ilipoanzishwa haijapata kuwa na
kompyuta hivyo msaada huo ni mkubwa kwao na kuomba wadau wengine
kuzidi kusaidia shule hiyo
0 comments:
Post a Comment