Home » » FAWE NA TUSEME KUMLILIA MTOTO WA KIKE

FAWE NA TUSEME KUMLILIA MTOTO WA KIKE

SHIRIKA la Forum For Africa Women Educationalists (FAWE) linalojihusisha na utoaji wa huduma za kielimu kwa mtoto wa kike, kupitia mradi wa TUSEME ambao huwawezesha wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kujitambua, kujiamini, kujithamini na kuzitete haki zao, limewakutanisha wanafunzi wa Wilaya tisa nchini, ili kubaini changamoto zinazowakabiri.
Akizungumza katika sherehe ya uzinduzi wa kambi ya wanafunzi hao, kambi iliyopo katika shule ya sekondari JJ Mungai katika Wilaya ya Mufindi mkoni Iringa, mratibu wa FAWE Tanzania Bi. Neema Kitundu amesema Wilaya zilizoshiriki katika kambi hiyo ni Temeke, Njombe, Mtwara, Mbeya Vijijini, Mufindi, Iringa vijijini pamoja na Makete, huku Wilaya ya Magu na Mbarali zikishindwa kuwapeleka wanafunzi wake katika shughuli hiyo.
Bi. Kitundu amesema lengo la shirika hilo ni kumuhamasisha mtoto wa kike aweze kupata elimu bora bila kukwamishwa na vizingiti vyovyote, kwa kumpa uthubutu wa kuchagua masomo ya Sayansi ili waweze kuingia katika taaluma mbalimbali kwa usawa baina yake na mtoto wa kiume, huku likijenga majengo yanayowezesha upatikanaji wa elimu bora, itolewe katika mazingira rafiki ya elimu kwa jinsia zote.
Mwanzirishi wa TUSEME nchini Profesa Penina Mlama amesema tangu kuanzishwa kwake mradi tayari umezifikia nchi 25 barani Afrika huku kukiwa na mafanikio makubwa katika utoaji wa haki ya elimu kwa mtoto wa kike.
Kaimu afisa elimu mkoa wa Iringa Mwalimu Ezekiel Kiagho amesema shirika hilo ni chachu katika sekta ya elimu, kutokana na ukweli kuwa baadhi ya wazazi na walezi wamekuwa wakiwabagua watoto wa kike katika afua ya elimu ikiwa pamoja na kumlimbikizia majukumu ya nyumbani na hivyo kukosa muda wa kujisomea.
Hata hivyo watoto washiriki Erick Kisima, Irene Nyavanga na Jennifer Steven Luvanda wamesema katika maeneo ya vijijini bado baadhi ya wazazi na walezi wanaendeleza ubaguzi kwa watoto wa kike katika suala zima la elimu, ikiwa pamoja na kumbebesha mzigo wa majukumu ya kazi za nyumbani.

1 comments:

JOHN said...

mwanamke ni mtu muhimu sana. Sina maana mwanaume hana umuhimu sana ila wote ni muhimu sana. tukijaribu kuangalia kwenye jamii tunaona mwanamke ndio yupo katika hali hasi karibu kila sehemu, mwanamke ndio mzazi anayelea mtoto, mwanamke anazalisha uchumi kuliko mwanaume. Tembea mashambani msimu huu halafu ujionee idadi ya wakulima na wanawake au wanaume. Kwahiyo kwa hayo machache naona mwanamke anatakiwa kupewa msaada mkubwa kutokana na hali halisi.

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa