Home » » SERIKALI YA MKOA WA IRINGA YAPONGEZA TUZO YA UBORA WA MAZIWA AFRIKA ILIYOPATA KAMPUNI YA ASAS DAIRIES LTD

SERIKALI YA MKOA WA IRINGA YAPONGEZA TUZO YA UBORA WA MAZIWA AFRIKA ILIYOPATA KAMPUNI YA ASAS DAIRIES LTD

Kaimu  mkuu wa mkoa wa Iringa Richard  Kasesela (wa tatu kushoto )ambae ni mkuu wa wilaya ya  Iringa akiongoza  washiriki wa warsha  ya  wiki moja ya kilimo  biashara  yaliyoandaliwa na  Shirika la umoja wa mataifa linalojishughulisha na kilimo (UNCTAD)  kwa ufadhili  wakampuni  ya Asas Dairies Ltd na  SAGCOT kupongeza ubora  wa maziwa ya kampuni ya  Asas Dairies Ltd  baada ya kushinda  tuzo ya ubora wa bidhaa  za maziwa Afrika  tuzo ya ARSO leo wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo ,wengine  pichani  kutoka kushoto  wa  kwanza ni  Meneja maendeleo na biashara  Roy Omulo ,mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Asas Dairies Ltd Ahmed Abri  na mwakilishi wa  katibu mtendaji wa SAGCOT CTF Mbosela John Mosela kulia
Kaimu  mkuu wa mkoa wa Iringa Richard  Kasesela ( mwenye suti katikati) akiwasili  eneo la  warsha  kwa ajili ya ufungaji  kushoto  kwake ni mkurugenzi wa Asas Dairies Ltd Ahmed Abri na  washiriki  wengine
Kasesela kulia  akiongoza wana  warsha  kupiga makofi
Kaimu  mkuu wa mkoa wa Iringa Richard  Kasesela (wa tatu kushoto )ambae ni mkuu wa wilaya ya  Iringa akiongoza  washiriki wa warsha  ya  wiki moja ya kilimo  biashara  yaliyoandaliwa na  Shirika la umoja wa mataifa linalojishughulisha na kilimo (UNCTAD)  kwa ufadhili  wakampuni  ya Asas Dairies Ltd na  SAGCOT kufungua maziwa kabla ya kupongeza ubora  wa maziwa ya kampuni ya  Asas Dairies Ltd  baada ya kushinda  tuzo ya ubora wa bidhaa  za maziwa Afrika  tuzo ya ARSO wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo ,wengine  pichani  kutoka kushoto  wa  kwanza ni  Meneja maendeleo na biashara  Roy Omulo ,mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Asas Dairies Ltd Ahmed Abri  na mwakilishi wa  katibu mtendaji wa SAGCOT CTF Mbosela John Mosela kulia
Kaimu  mkuu wa mkoa wa Iringa Richard  Kasesela (katikati)ambae ni mkuu wa wilaya ya  Iringa akifunga warsha ya  wiki moja ya kilimo  biashara  yaliyoandaliwa na  Shirika la umoja wa mataifa linalojishughulisha na kilimo (UNCTAD)  kwa ufadhili  wakampuni  ya Asas Dairies Ltd na  SAGCOT kwa  wafugaji 35 kutoka mkoa wa Iringa , Mbeya na Njombe leo ,kushoto wa kwanza ni meneja biashara na maendeleo  wa kampuni ya maziwa  ya Asas akifuatiwa na mkurugenzi wa kampuni ya Asas Dairies Ltd Ahmed Abri na kulia  ni mwakilishi wa  katibu mtendaji wa SAGCOT CTF Mbosela John Mosela
Kasesela  akimnyoshea  kidole mkurugenzi wa Asas Dairies Ltd  Ahmed  Abri  wakati akipongeza jitihada  zao
Mkurugenzi wa Asas Dairies Ltd  Ahmed Abri  akifurahia hotuba ya Kasesela
Washiriki wa warsha hiyo wakifuatilia  hotuba ya Kasesela
Kasesela  akiwa katika  picha ya pamoja na mkurugezi wa Asas Dairies Ltd Ahmed Abri (katikati) na Ahmed Bin Is Haq
wawakilishi wa taasisi  za kifedha Iringa  wakiwa katika  warsha  hiyo
Mwakilishi  wa Finca  akieleza aina  ya mikopo  iliyopo
washiriki wa warsha  hiyo
Kaimu  Rc Iringa Richard  Kasesela  akigwa  vyeti kwa washiriki wa warsha  hiyo
Mshiriki Asha Lukasa kutoka  kikundi cha Syukula Kisegese Tukuyu  akipozi na kaimu RC Iringa Richard Kasesela baada ya  ukupewa  cheti  chake  cha ushiriki
Na MatukiodaimaBlog
SERIKALI  ya  mkoa  wa  Iringa  imeipongeza kampuni ya  maziwa ya Asas Dairies Ltd ya  mkoani Iringa  kwa kushinda tuzo  ya (ARSO) kwenye  mashindano ya  kimaifa ya nchi  za Africa ya  ubora  wa bidhaa za maziwa   kuwa ni tuzo yenye heshima kubwa kwa mkoa huo na Tanzania kwa ujumla .

Pamoja na pongezi hizo  pia imepongeza  jitihada  zinazofanywa na kampuni ya  Asas Dairies  Ltd  kwa  kuwawezesha mafunzo  mbali mbali wafugaji  wa mikoa ya Mbeya , Njombe na  Iringa  kubadili  ufugaji wa  kienyeji na  kufuga  kibiashara  zaidi  .

Huku  ikiwataka wenye  viwanda  vya  usindikaji  maziwa kujenga utamaduni  wa  kuwafikia  wafugaji na  kuwapa   elimu  ili  kuwezesha  bidhaa zao  za maziwa  kuendelea   kuwa  zenye  ubora  zaidi  na  ikiwezekana  kuwawezesha  kupata vifaa vya  kisasa  vya  kukamulia maziwa.

Kaimu  mkuu  wa  mkoa wa Iringa Richard Kasesela  aliyasema hayo leo  kwenye ukumbi wa Asas mjini hapa  wakati wa  ufungaji wa mafunzo ya wiki moja kwa wafugaji 35  kutoka Iringa , Mbeya  na Njombe  mafunzo yaliyoandaliwa kilimo  biashara  yaliyoandaliwa na  Shirika la umoja wa mataifa linalojishughulisha na kilimo (UNCTAD)  kwa ufadhili  wakampuni  ya Asas Dairies Ltd na  SAGCOT  CTF


Alisema kuwa kampuni  hiyo  imeupa mkoa wa Iringa  heshima  kubwa na kuwa ukiacha mashindano mbali mbali ya maziwa kwa viwanda  vya ndani ya  Tanzania kampuni  hiyo imekwisha  shinda mara nne  sasa jambo ambalo ni la kujipongeza na kujivunia kuwa bidhaa  zinazozalishwa ni bora na hivyo si wakati wa watanzania  kukimbilia bidhaa za nje na kuacha zinazozalishwa ndani ya nchi .

Kasesela ambae  pia ni mkuu wa wilaya  ya Iringa  alisema kuwa mbali ya  wadau na wawekezaji  waliopo katika wilaya  yake na mkoa wa Iringa  wamekuwa msaada katika maendeleo  ila bado kampuni  hiyo ya  Asas Dairies Ltd  imekuwa ni msaada  zaidi si tu kwa mambo ya  serikali bali hata katika kuwawezesha   wakulima na  wafugaji   kupatiwa elimu .

Alisema  ni  vema  wamiliki  wa  viwanda   kuwa na mbinu ya  kuwafikia  wafugaji na  kuwapa  elimu na  mbinu ya  kuongeza kasi  ya uzalishaji wa maziwa  bora   ili  kuviwezesha   viwanda  vyao  kuwa na maziwa  mengi  zaidi na  bora  na  sio  bora  maziwa .

Kuwa  serikali  ya mkoa wa Iringa  inatambua  faida ya mafunzo hayo kwa  wafugaji na pia  jitihada za wahisani  mbali mbali  wakiwemo SAGCOT ,Asas Dairies Ltd   na wengine  na kuwa  jitihada  hizo  zinafanywa na SAGCOT kwa makubaliano ambayo yamefikiwa kati yao na  serikali ya awamu ya tano kwa  lengo la kuwakomboa  wakulima wadogo na wafugaji .
Hivyo  aliwataka  wafugaji hao ambao  wamepewa  elimu   hiyo  kwenda kuitumia   vizuri  ili  kufanikisha azma ya  serikali ya awamu ya tano kwa  kuona  kilimo  na ufugaji  inakuwa ni  fursa nzuri ya  kumkomboa  mwananchi .

Kasesela  alisema kuwa kwa  mujibu wa tafiti  inaonyesha  kasi ya  watanzania  kunywa maziwa  bado  ni ndogo  sana  kuliko  unywaji wa pombe jambo   hali  ambayo ni hatari  kwa afya   na hivyo ni vema  kuendelea  kuhamasisha  wananchi  kunywa maziwa  zaidi  kwa afya  zao  kuliko pombe ambazo  kimsingi  kiafya hazina  faida  yeyote  mwilini .

Mkurugenzi  wa kampuni ya  Asas Dairies  Ltd   Ahmed Abri  kampuni   yake  ilianza  mwaka 2000 kwa  kuanza  kusindika  maziwa  kati ya  lita 1000 – 1500 kwa  kutengeneza maziwa mgando  na maziwa halisi baada  kuoa  bidhaa hiyo  inahitajika  zaidi mjini Iringa  walazizimika  kuanza  kukusanya maziwa kutoka maeneo mbali mbali ukiacha yale  ambayo  yalikuwa  yakitoka  shambani kwao .

“ Tuliamua  kuanza  kuwatembelea  wafugaji maeneo mbali  mbali  na  mwaka 2005 -2006  idadi ya  wafugaji  iliongezeka  zaidi  kufikia  wafugaji  43 hivyo  kuanza  kutengeneza  bidhaa mpya ya  Yoghurt ila bado chagamoto  ilikuwa ni maziwa hivyo  kulazimika kwenda  nje  ya mkoa wa Iringa kama Njombe na Mbeya wilaya ya Rungwe  na  kuwa kiwanda  chetu  kilikuwa na uwezo wa kuzalisha maziwa lita 50,000 kwa siku   kutoka  lita 12,000 “

Abri  alisema kwa  sasa baada ya  kutoa  elimu mbali mbali kwa mikoa ya Iringa ,Njombe na Mbeya  hivi sasa  kiwanda  hicho  kinawafugaji  1800 ambao wanapeleka maziwa hapo .
Aidha  alisema  wakati shirika la afya Duniani linasisitiza kila binadamu  kunywa maziwa lita 200 kwa mwaka  ila kwa  watanzania  hata  lita  mbili kwa mwaka mtu  hanywi maziwa na kama atakunywa kwa  wingi  basi ni baada ya  kuandikiwa na daktari .

“ Sisi  kama kama kampuni  tumekuwa tukihamasisha  unywaji wa maziwa na  kila mwaka  tumekuwa  tukihamasisha mashuleni  na lengo kuona  watanzania  wanajenga utamaduni wa kupenda  kunywa maziwa zaidi kwani Tanzania kwa siku  inazalisha maziwa  lita  300,000 pekee ambazo haziishi sokoni kutokana na watu  kutopenda  kunywa maziwa  huku Kenya  inazalisha maziwa lita milioni moja  kwa  siku na bado  wanalalamika  haziwatoshi .

Kuwa maziwa yanayozalishwa nchini ni lita kama 100,000 pekee  ndizo  zinapelekwa kiwandani na maziwa yanayobaki  yanauzwa  mitaani ambayo hayana  ubora hivyo rai  yao kwa watanzania ni  kupenda  kunywa maziwa yaliyosindikwa kutoka  viwandani  kuliko  kunywa maziwa yasiyo na ubora  yanayozungushwa mitaani .

Abri  alisema kutokana na kuzingatia ubora  wa maziwa na  wafugaji  kuzalisha maziwa  bora  kampuni  ya  Asas Dairies Ltd imeendelea   kuongoza nchini   kwa  kushinda  tuzo  za  ubora  wa bidhaa zake kwa miaka minne mfululizo na mwaka  huu imeshinda tuzo nyingine ya mashindano ya  kimaifa ya nchi  za Africa  tuzo ya ARSO  yaliyofanyika Julay  mwaka  huu mjini  Arusha  yaliyoshinisha makampuni zaidi  ya 60 toka ndani na nje .





0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa