Home » » DC KILOLO ASHIRIKI KUFYEKA VICHAKA NA NYASI NDEFU NJE YA OFISI YAKE ,AONYA WATAKAOSHINDWA KUFANYA USAFI

DC KILOLO ASHIRIKI KUFYEKA VICHAKA NA NYASI NDEFU NJE YA OFISI YAKE ,AONYA WATAKAOSHINDWA KUFANYA USAFI

Mkuu  wa  wilaya  ya  Kilolo Bi Asia  Abdalah  akishirikiana na  wanafunzi  wa  shule  ya  Sekondari Kilolo  kufanya  usafi  wa  kufyeka  nyasi nje  ya  ofisi ya  mkuu  huyo wa  wilaya  juzi kama  sehemu ya  kuitikia agizo la  Rais Dr John Magufuli la  kila jumamosi ya  mwisho  wa mwezi  ni  siku ya  usafi
Jengo  la ofisi  la ofisi ya  DC Kilolo
Kaimu  mkurugenzi  wa  Halmashauri ya  Kilolo  akishiriki  usafi nje ya  ofisi ya  DC  Kilolo
Watumishi  Kilolo  na  wanafunzi   wakifanya  usafi  ofisi ya  mkuu wa wilaya ya  Kilolo mkoani Iringa
Mkuu  wa  wilaya  ya  Kilolo Bi Asia Abdalah  na  wakuu wa   idara  katika  Halmashauri ya Kilolo  wakiwa  wameungana na  wanafunzi  wa  shule  ya  sekondari  Kilolo  kusafisha  mazingira  yanayozunguka  ofisi ya  mkuu  wa wilaya ya Kilolo
DC  Kilolo  akishiriki  kufyeka  vichaka na majani  yaliyokuwepo nje ya  ofisi  yake
Usafi  nje ya  ofisi ya  DC  Kilolo
Mtumishi  wa Halmashauri ya  Kilolo  akichoma moto nyasi  zilizokusanywa
Mkazi  wa Luganga  Kilolo  akishiriki  kufanya  usafi  kuzunguka  nyumba  yake  kama  sehemu ya  kuitikia  wito  wa mkuu  wa  wilaya ya  Kilolo
DC  Kilolo  akishiriki  usafi na  wanafunzi  wa  shule ya  msingi  Kilolo
DC  Kilolo  akiwapongeza  wananchi  wa watumishi  Kilolo kwa  kujitokeza  kufanya usafi
DC  Kilolo  Bi  Asia  Abdalah  akiwa na wanafunzi wa baadhi ya  watumishi wa Kilolo walioshiriki  usafi
Na MatukiodaimaBlog 
MKUU  wa  wilaya  ya  Kilolo Asia Abdulah ametangaza  kuwachukulia  hatua  kali  wananchi  watakaopuuza agizo la   Rais Dr  John Magufuli na   kufanya usafi  wa mazingira  yanayowazunguka  kila juma  la mwisho la mwezi .

Huku  akipiga  marufuku   kilimo  cha mahindi nje  ya ofisi  yake  kuwa kuendelea  kulima mahindi na mazao yanayozidi  futi tatu  katika eneo   linalozunguka  ofisi  yake ni moja ya  uchafuzi  wa mazingira na  kuwa kuanzia   sasa mazao marefu katika  maeneo yote  yanayozunguka ofisi za  umma  ni marufuku .

Mkuu  huyo  wa  wilaya alitoa kauli  hiyo  juzi  baada ya  kuongoza oparesheni  ya usafi kwa watumishi  wa Halmashauri ya  Kilolo na wanafunzi  wa   shule ya sekondari  Kilolo  kufanya usafi maeneo ya jengo la  ofisi  ya  mkuu  wa   wilaya ya  kilolo  jengo  ambalo nyoka walikuwa wakitishia usalama  wa  watumishi  wa  ofisi  hiyo  kutokana na jengo   hilo  kuzungukwa na  nyasi  ndefu na  vichaka kwa  zaidi ya miaka 10 .

Akizungumza  baada ya  zoezi  hilo  mkuu  huyo  wa  wilaya  aliwapongeza  wakuu  wa idara  katika halmashauri ya  Kilolo pamoja na  wananchi  ambao  waliitikia  wito  wa  kufanya  usafi    huku  akisema  idadi ya  wananchi  waliofika  kufanya  usafi  hajafurahishwa nao  kwani  ni  wananchi  wachache  ambao   walitoka  kufanya  usafi  pamoja na  gari ya matangazo   kupita  mitaani kabla  ya  siku ya  usafi  na  kuhamasisha  wananchi  kushiriki zoezi hilo .

“Wakati nikifika wilayani hapa na kuanza majukumu yangu  mapya takribani mwezi mmoja uliopita kwa kweli sikuridhishwa na hali ya usafi wa mazingira haya  ya ofisi .....nimelazimika  kuanza  usafi kwanza  hapa  ofisini  kwangu  maana  ni hatari hata kwa  usalama kama  nyoka  na wadudu  wengine...hii  ni  serikali ya  hapa  kazi  Tu hivyo kama  mheshimiwa rais  wetu mpendwa Dr John Magufuli  alishiriki mwenyewe   usafi hivyo ni lazima kila mmoja  kuonyesha  kuunga mkono kwa  vitendo na sitaacha  kuchukua  hatua  kwa  wote  watakaoshindwa  kufanya  usafi  ,”

Bi  Asia  alisema  kuwa  kutokana na zoezi  hilo  kuwalenga  wananchi  wote kwa  kila mmoja kufanya  usafi katika   eneo  lake analo ishi  kwa  upande  wake hakuona  sababu ya  kuanza  kuhamasisha  wananchi  kufanya  usafi kwenye mazingira  ambayo yanawazunguka   wakati  mazingira  yanayozunguka   ofisi  yake mkuu  wa  wilaya  kuwa machafu hivyo  alilazimika   kuhamasisha   wakuu wa idara  na  walimu pamoja na  wanafunzi   kufika  kusaidia   kuweka mazingira  safi katika   ofisi  hiyo .

Pia  alisema atawashauri  madiwani  kutunga  sheria  ndogo za  usafi  wa mazingira  itakayotumika  kuwawajibisha wananchi watakaoshindwa  kufanya  usafi  katika maeneo  yao na kwa  kuanza anawataka   wananchi  wote  wa wilaya ya  Kilolo kuacha tabia  ya  kupanda mahindi kando  ya  nyumba  zao  kwani  ni hatari  kwa usalama  wao .

Hata   hivyo  alisema utamaduni  wa  wananchi  kushiriki uchafu  umekuwa ni mdogo  sana katika  wilaya   hiyo hasa  ukitokana na mazoea yakutoshirikishwa zoezi  hilo la  usafi ambalo  alisema kwa  sasa usafi  wa mazingira  si kujitakia  tena ni lazima kwa  wananchi  wote  kufanya  usafi  katika maeneo  yao kila   jumamosi ya mwisho  kwa kila  mwezi na atakayepuuza atawajibika kwa   mujibu wa  sheria .

Baadhi  ya  wananchi  walioshiriki  usafi  katika  ofisi  hiyo ya  mkuu  wa  wilaya  walieleza  kufurahishwa na hatua ya  mkuu  huyo  wa  wilaya  kuonyesha mfano  wa  vitendo  kwa  kuanza  usafi  katika mazingira  yanayozunguka  ofisi  yake ambayo yalikuwa ni machafu zaidi ukilinganisha  na mazingira  yanayozunguka ofisi  nyingine ama  makazi  ya  wananchi .


Salome Kikoti  ni mkazi  wa  Lugalo  alisema  kuwa mwonekano  wa mazingira ya  ofisi ya  mkuu  wa wilaya  yalikuwa ni mabaya  zaidi na kuwa hata  watumishi  wa ofisi   hiyo walikuwepo hatarini  kung'atwa na nyoka .


" Leo  wakati  tunafanya  usafi  wa  kufyeka nyasi na  vichaka katika eneo  hili la ofisi ya mkuu  wetu wa wilaya tumeua  nyoka  mmoja hii ni dalili  ya  wazi  kuwa  kuendelea  kuviacha  vichaka   hivi  na  uchafu katika mazingira  haya ya ofisi ya mkuu wa  wilaya  ilikuwa ni  kukaribisha  nyoka  kuweka makazi  yao eneo hili "


Pamoja na  mkuu  huyo wa  wilaya  kufanya  usafi katika  ofisi  yake  pia  alishiriki  kufanya  usafi Zahanati  ya Kilolo ,shule ya  msingi  Kilolo na katika maeneo ya  biashara  ya  wananchi  wa Luganga Kilolo .

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa