Home » » TUKIO KATIKA PICHA: INASIKITISHA. BASI LA NGANGA NA FUSO ZATEKETEA KWA MOTO BAADA YA KUGONGANA LEO

TUKIO KATIKA PICHA: INASIKITISHA. BASI LA NGANGA NA FUSO ZATEKETEA KWA MOTO BAADA YA KUGONGANA LEO





unnamed (63)basi hilo baada ya kupata ajali ya kuungua.
Habari zilizotufikia muda huu wa saa nane mchana ni kuwa hadi sasa imeelezwa kuwa watu sita (6) wamepoteza maisha kufuatia ajali ya basi la abiria la Nganga lililogongana na Fuso, na kupelekea magai hayo kuwaka moto, katika eneo la Ruaha Mbuyuni mpakani kwa Morogoro na Iringa.
Hata hivyo, bado kuna ugumu wa habari kamili kutokana na umbali wa eneo hilo la tukio huku tukihalifiwa kuwa, makamanda wa jeshi la Polisi wa Morogoro na Iringa wote simu zao hazipatikani kwa muda mrefu. Ambapo pia kutokana na ufinyu wa bajeti kwa baadhi ya vyombo vya habari, wameshindwa kufika kwa wakati kwenye eneo la tukio kutokana na kuwa mbali na miji mikuu ya mikoa hiyo ya Iringa na Mbeya.
Kwa mujibu wa ripota wetu kutoka Mkoa wa Morogoro alibainisha kuwa, karibu wandishi wengi wameshindwa kuelekea eneo la tukio kutokana na vyombo vyao kutokuwa na mafuta ya kutosha huku hapo hapo Ofisi za jeshi hilo la Polisi kwa siku ya leo nyingi zikiwa zimefungwa.
MODEWJI: Hallo!!: Hapo Morogoro tupeni Habari. vipi kuhusiana na ajali ya Ruaha Mbuyuni!.
RIPOTA MOROGORO: “Ni kweli lakini  sote tunataka kwennda lakini tumeshindwa huko ni mbali sana.. kutoka hapa Morogoro Mjini hadi hapo ni zaidi ya KM110 ambazo tu unaimaliza mbuga ya Mikumi, ukitoka hapo uanze kuitaafuta Mbuyuni ni zaidi ya KM 35, hivi?.
Unafikiri ni karibu? tumeshindwa hata magari ya abiria tunayoomba lifti, kwa muda huu tutachelewa tu”. Kilieleza chanzo hicho.
Chanzo hicho pia kilibainisha kuwa, kutokana na ajari hiyo kutokea katikati ya mpaka wa Morogoro na Iringa, majeruhi wanaweza kupelekwa Hospitali iliyopo Mikumi ama Iringa mjini.
Modewji ilipowasiliana na ripota wa kujitegemea Mkoani Iringa, alibainisha kuwa,  hadi sasa bado wanaendelea kukusanya taarifa ila walioweza kupoteza maisha hapo hapo ni sita, akiwemo pamoja na dereva wa Fuso.
Picha ambazo zimeweza kupatikana ni kwa msaada wa  teknolojia ya simu za kisasa zenye uwezo wa kupiga picha na kurusha kwa kutumia intaneti (tehama/ICT) hivyo tunapongeza kwa teknolojia hii na kwa wale walioweza kutuma picha hizi ambazo kwa asilimia kubwa hazikukiuka maadili. ..credit ziende kwa waliopiga hizi picha za ajali, Pia Modewji blog inatoa pole kwa wale wote walioondokewa na wapendwa wao, waliojeruhiwa na kupata matatizo kwenye ajali hiyo.
Modewji blog, tunaendelea kuwasiliana na vyanzo zaidi ilikukupatia abari iliyo bora, endelea kuperuzi nasi. 
HABARI KWA HISANI YA MO BLOG


Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa