Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Atufigwege Kasesela akizungumza na mmoja wa watoto wanaolelewa katika kituo cha kulea watoto wenye ulemavu kiitwacho Nyumba Ali kilichopo Wilolesi, Wilayani Iringa.
Kituo kimoja kinapokea watoto 35. Wamekuwa wanawafanyia mazoezi ya viungo pamoja na kuwafundisha kazi za mikono mbalimbali watoto wenye ulemavu wa viungo na akili.
Katika kituo hiki yupo mtoto aitwaye Zawadi ambaye amesomeshwa hadi kiwango cha darasa la saba, Mtoto huyu hawezi kutumia mikono anatumia miguu kwa shida akisaidiwa na kompyuta na amefanikiwa kuandika kitabu kinacho elezea maisha yake.
Jumamosi,
Julai 15, 2017 Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Atufigwege Kasesela
alitembelea kituo cha kulea watoto wenye ulemavu kiitwacho Nyumba Ali
kilichopo Wilolesi. Nyumba Ali iliundwa na umoja wa wazazi wenye watoto
waishio na ulemavu mkoani Iringa.
Lengo
la kuunda umoja huo ulikuwa ni kuwakutanisha wazazi ili waweze kuwa na
sauti moja katika kubainisha na kusaidiana katika kutatua changamoto
mbalimbali zinazo ikumba jamii ya watoto waishio na ulemavu. Akitoa
taarifa Mbele ya Mkuu wa wilaya mratibu wa kituo hicho, Adam Duma
alisema wamefungua vituo hivyo viwili kimoja kikiwa Wilolesi na kingine
Ngome.
Akizungumza
na wazazi na walezi wa kituo hicho, Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard
Kasesela alisema “ Nasikitishwa na baadhi ya wazazi ambao wanajaliwa
kupata watoto wenye ulemavu na kuwatelekeza hili halikubaliki.
Kila
afisa tarafa afanye utafiti nyumba hadi nyumba kubaini kama kuna mtoto
mlemavu, Nachukia sana tabia ya baadhi ya wakina baba kukimbia watoto
wenye ulemavu na kuwachia wakina mama. Hebu wanaume tuache tabia ya
kukimbia watoto wenye ulemavu.” alisema. Pia aliwataka wakina baba
wajitokeze kufika kwenye kituo sio kuwachia wakina mama peke yao.
0 comments:
Post a Comment