Mkuu wa wilaya ya Iringa Bw Kasesela akisalimiana na Geofrey Mungai kulia |
Bw Mungai akiwa na mmoja kati ya watoto yatima wanaolelewa kituo cha DBL |
Mtoto wa mbunge Mwamoto Leah akitoa ahiadi yake ya Tsh 50000 kwa ajili ya kusaidia yatima |
katibu wa CCM Iringa mjini akiahidi kuchangia yatima hao |
Mbunge Kabati akiahidi kuchangia Tsh 500,000 kwa ajili ya Yatima hao Na MatukiodaimaBlog WATOTO yatima wa kituo cha Daily Bread Life Ministres cha Mkimbizi katika Manispa ya Iringa na wale wa kituo cha Tosamaganga katika wilaya ya Iringa Iringa wapewa msaada wenye nguo na chakula msaada wenye thamamani ya Tsh milioni 3 kwa ajili ya sikukuu ya Chrismas na mwaka mpya .pamoja na msaada huo wa chakula na mavazi pia Mungai aliahidi kuchangia Tsh milioni 1.5 kwa ajili ya ununuzi wa vyombo vya muziki katika kituo hicho na kufanya msaada wake kufikia Tsh milioni 4.5
Huku
mkuu wa wilaya ya Iringa Richard Kasesela pamoja na kumshukuru
mfanyabiashara huyo kwa kukumbuka yatima bado ametoa onyo kali kwa
wanawake wote wanaotupa watoto kuwa ikibainika watachukuliwa
hatua kali .
Akizungumza
baada ya kukabidhi msaada huo Geofrey Mungai alisema imekuwa ni
kawaida ya familia yake kila mwaka kusherekea sikukuu mbali
mbali pamoja na watoto yatima kama sehemu ya kuikumbusha jamii
kuwa na utamaduni wa kuwatazama yatima hao ambao tegemeo lao kubwa
ni jamii inayowazunguka.
Mungai alisema kuwa suala la
kulea yatima linapaswa kuwa ni jukumu la watanzania wote na kuwa ili
kuwawezesha watoto hao kujisikia ni sehemu ya familia zenye wazazi ni
vema jitihada za vituo vya yatima hapa nchini kuendelea kuheshimika
zaidi.
Hata
hivyo Bw.Mungai alisifu kazi nzuri inayofanywa na kituo hicho cha DBL
katika kuendelea kuwalea watoto ha kimwili na kiroho na kuendelea kuwa
miongoni mwa vituo bora vya kulea yatima katika mkoa wa Iringa.
Aidha
aliwataka wananchi wengine kuendelea kufika katika kituo hicho na
kusaidia kulea watoto hao kwa kutoa misaada mbali mbali kama njia ya
kuwafariji na kuwalea watoto hao kuliko kuwaachia walezi wao pekee.
Hivyo
alisema kwa mwaka huu amelazimika kutoa msaada wa nguo na
chakula kwa kila kituo msaada wenye thamani ya Tsh milioni 1.5 na
kuwa ataendelea kufanya hivyo kwa ajili ya watoto hao ili siku
ya sikukuu nao waweze kufafana na watoto wengine ambao
wanawazazi wao wote wawili .
Mkurugenzi
mkuu wa kituo hicho mchungaji Mpeli Mwaisumbe
Bw. Tukuswiga Mwaisumbe alisema kuwa kituo chake cha DBL kilichopo
chini ya usimamizi wa mchungaji Neema Mwaisumbe kina watoto yatima
43 na kuwa maendeleo ya kituo hicho yametokana na jitihada za
wadau mbali mbali ambao wameendelea kujitolea kusaidia kituo hicho.
Alisema
kuwa mbali ya familia hiyo ya Mungai kuendelea kutoa msaada wakati wa
sikukuu mbali mbali kwa watoto hao bado michango yake imeendelea kuwa
chachu kwa wadau wengine kujitokeza kusaidia watoto hao kwa misaada mbali mbali .
Hata
hivyo alisema kuwa wadau wanaoendelea kusaidia kituo hicho ni wengi
zaidi na kuwa kwa umoja wao kituo hicho kinaendelea kuthamini michango
yao na kuomba kuzidi kujitolea zaidi kwa ajili ya watoto hao kwa ajili
ya kuona watoto hao wanapata elimu Kituo hicho ambacho kina zaidi
ya miaka 15 15 toka kuanzishwa
kwake kimefanikiwa kuanzisha shule yake ya Sekondari iliyopo
kijiji cha Mgera ambayo inapokea na watoto wengine kwa kuchangia ada
ndogo zaidi kuzindua shule ya sekondari .
kama
umeguswa na jitihada za wale wote wanaojitolea kusaidia yatima wa kituo
hiki cha DBL mkimbizi Iringa unaombwa kuchangia mchango wako wowote
kupitia namba hii ya mkurugenzi mtendaji wa kituo hiki mchungaji Mpeli
kupitia huduma ya TIGO PESA 0719239936 na M-PESA ni 0754362536 na Mungu atakubariki na kukuongezea pale ulipopunguza.
Aidha
alishukuru ushirikiano kubwa ambao umekuwa ukionyeshwa na wadau
mbali mbali kama mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu
ambae amekuwa akijitolea kusomesha baadhi ya watoto elimu ya msingi
kwenye shule yake ya Star pia mbunge wa viti maalum mkoa wa
Iringa Ritta Kabati (CCM) na mkuu wa wilaya ya Iringa Richard
Kasesela pamoja na wadau wengine mbali mbali .
Kwa
upande wake mkuu wa wilaya ya Iringa Kasesela alisema kuwa
hatapenda kuona katika wilaya yake watoto wanaendelea kutupwa ama
kutelekezwa na wazazi wao baada ya kuzaliwa na kutaka wananchi
kutoa ushirikiano kwa kuwafichua wale wote wanaotupa watoto .
Mkuu
huyo wa wilaya kwa kushirikiana na mbunge wa viti maalum mkoa wa
Iringa Ritta Kabati (CCM) kwa ajili ya kuungana na Mungai kusaidianbsp;
watoto hao walichangia Tsh milioni moja
|
0 comments:
Post a Comment