Home » » MWIMBAJI AMBWENE MWASONGWE NA KWAYA YA VIJANA KKKT IRINGA MJINI KUPAMBA SIKU YA MAM HALL MAFINGA

MWIMBAJI AMBWENE MWASONGWE NA KWAYA YA VIJANA KKKT IRINGA MJINI KUPAMBA SIKU YA MAM HALL MAFINGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Image result for Mwimbaji Ambwene  Mwasongwe
Mwimbaji  Ambwene Mwasongwe
Mbunge   wa jimbo la  Kilolo Bw  Venance Mwamoto  katikati aliyevaa tai akiwa na mbunge wa viti maalum  mkoa wa Iringa Ritta Kabati katika  picha ya  pamoja  na waimbaji wa kwaya ya  vijana  KKKT dayosisi ya  Iringa walipotembelea  bunge Juni 8 mwaka  huu 
Na  MatukiodaimaBlog 

MWIMBAJI wa nyimbo za injili maarufu nchini Ambwene Mwasongwe  na kwaya maarufu ya  vijana  wa kanisa  kuu la kiinjili la kilutheri Tanzania (KKKT) usharika  wa Iringa mjini   ambayo ni washindi wa pili kiuimbaji Taifa kunogesha tamasha  la  uimbaji   litakalosindikiza  uzinduzi wa ukumbi wa Mam mjini Mafinga .

Mratibu wa tamasha  hilo  Mary Mungai  alisema  kuwa  tamasha hilo kubwa la uimbaji limepangwa  kufanyika Desemba 26 mwaka huu ambalo   itakuwa ni  siku ya kusherekea sikuuu ya Chrismas  ,kutakuwa na  waimbaji mbali mbali kutoka ndani ya mji wa Mafinga ,nje ya Mafinga   na kutoka Dar es Salaam .

Alisema  mbali ya  mwimbaji Mwasongwe na kwaya ya  vijana  kutoka  Iringa mjini ambayo ni kwaya  inayofanya  vizuri katika  nyimbo  za injili hapa nchini pia  kutakuwa na  waimbaji  wengine mbali mbali pamoja na burudani nyingine na  kuwa  lengo  la tamasha  hilo  pamoja na kutoa  burudani kwa  wakazi wa wilaya ya Mufindi na mikoa ya Iringa  na Njombe  bado itakuwa ni  siku ya MAM Hall itakayokwenda  sanjari na  uzinduzi wa   ukumbi wa  burudani na sherehe mbali mbali katika mji huo .
Hivyo  alisema  kwa ajili ya  kuwashukuru  wananchi wa mji  wa Mafinga  kwa ushirikiano mbali mbali ambao  wameendelea  kuutoa amelazimika  kuandaa tamasha hilo ambalo  wananchi  watashuhudia  kwa  kiingilio kidogo  sana  kama  sehemu ya kuchangia  gharama ndogo ndogo  za  maandalizi ya  tamasha .

Hivyo  alisema   mchango kwa  V.I.P  utakuwa ni Tsh 10,000  wakati kawaida kwa  watu  wazima ni Tsh 5000 na watoto ni Tsh 3000 pekee  na  kuwa  ili  kuepusha  msongamano mlangoni tiketi zitaanza kuuzwa  Desemba 15 katika  ofisi ya  shule ya Southern Highlands Mafinga , Hazina Bima na  Stationary ya Huruma Msigala

Akielezea  kuhusiana na ukumbi huo  alisema ni  ukumbi pekee katika mikoa ya nyanda za  juu kusini kujengwa  kisasa na utakuwa na majukwaa mawili  moja la kati  litakuwa ni  jukwaa  linalotembea pia  kutakuwa na V.I.P kwa wageni maalum ambao ili  waweze  kuingia ukumbini watapandishwa ghorofani  kwa ngazi maalum  za umeme na  kushuka kwa  ngazi hadi  jukwaani iwapo watataka  kutoingilia mlango wa waalikwa  wote .

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa