Home » » WAZIRI WILLIAM LUKUVI ATEMBELEA NYUMBA ZILIZOHAMISHIWA UMILIKI TOKA SHIRIKA LA NYUMBA KWENDA SERIKALI ZA MITAA MKOANI IRINGA

WAZIRI WILLIAM LUKUVI ATEMBELEA NYUMBA ZILIZOHAMISHIWA UMILIKI TOKA SHIRIKA LA NYUMBA KWENDA SERIKALI ZA MITAA MKOANI IRINGA

1w
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi akijadiliana jambo na Kaimu Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa- Iringa, Repson Joshua wakati Waziri huyo alipofanya ziara mkoani humo na kupewa taarifa ya utendaji kazi wa Shirika baadaye kufanya ziara ya kutembelea nyumba zilizokuwa za NHC zamani na kukabidhiwa kwa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa baadaye kurejeshwa Serikali Kuu na akakutana na wapangaji waliokuwa wamepanga kwenye nyumba hizo.
Waziri alikusudia kuona hali alisi ya nyumba zilizopo Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, ili kupata taswira ya nyumba zote zilizoko Mikoa mingine na kutoa taarifa ya Mheshimiwa Rais juu ya mustakali wa nyumba hizi.
2s
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi akisalimiana na wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa- Iringa wakati Waziri huyo alipofanya ziara mkoani humo na kupewa taarifa ya utendaji kazi wa Shirika baadaye kufanya ziara ya kutembelea nyumba zilizokuwa za NHC zamani na kukabidhiwa kwa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa baadaye kurejeshwa Serikali Kuu na akakutana na wapangaji waliokuwa wamepanga kwenye nyumba hizo.
3s
Waziri Lukuvi, akiteta jambo na Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa William Donald Mafwele alipowasili ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa na baada ya hapo msafara uliojumuisha watendaji kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wa Mkoa Iringa ulielekea eneo la barabara ya Kalenga kuliko na nyumba 49. Mheshimiwa Waziri alifanya ukaguzi wa eneo hilo na kumuuliza Mkurugenzi wa Halmashauri, William Donald Mafwele kuhusu hali ya umiliki ulivyo sasa. Baada ya hapo msafara wa Waziri ulielekea eneo la Barabara ya Pawaga kuliko na nyumba 25.
4s
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi akionyeshwa ramani ambapo nyumba zilizorudishwa TAMISEMI zilipo.
5s
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi, akimsikiliza maelezo toka kwa Mpima Ardhi wa Manispaa ya Iringa Mwenda.
6s
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi, akizungumza na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa, Alex Boniphace Kimba.
7s
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi, akisikiliza kero za wapangaji waliopanga nyumba zilizokuwa Shirika.
8s
Wapangaji waliopanga kwenye nyumba zilizokuwa za NHC na kukabidhiwa kwa Manispaa ya Iringa wakimsikiliza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Vangimembe Lukuvi (hayuko pichani) kwenye ukumbi wa Mwembetwoga mkoani Iringa.
9s
Kaimu Meneja wa Shirika la Nyumba Taifa mkoani Iringa, Repson Yosia akisoma taarifa mbele ya Mheshimiwa Waziri.
10s
Kaimu Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa mkoa wa Iringa akimkabidhi taarifa Mheshimiwa Waziri.
11s
Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa, William Donald Mafwele akisoma taarifa mbele ya Mheshiwa Waziri.

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa