RC Iringa Amina Masenza
......................................................................
Na MatukiodaimaBlog
Ndugu Wananchi wa Mkoa Iringa,
Ndugu Waanishi wa Habari,
Mabibi na Mabwana.
Nachukua
fursa hii kueleza umma kwa muhtasari utekelezaji wa ilani ya ccm ya mwaka 2015
kwa kipindi cha januari hadi juni, 2016 katika Mkoa wa Iringa.Taarifa hii ni
sehemu ya utekelezaji ambayo ilianza mwaka 2015.
Ndugu Wananchi, shughuli
zilizo tekelezwa kwa kipindi hicho zimefanikishwa kwa kuunganisha nguvu za
Serikali kuu,Serikali za Mitaa,Wahisani mbalimbali,Sekta binafsi, Wananchi
wenyewe na Mashirika yasiyo ya Kiserikali.Tunawashukuru wadau wote kwa michango
yao.
Ndugu Wananchi, Taarifa
hii imetoa maelezo ya utekelezaji na mafanikio yaliyopatikana kwa kipindi
husika kama ifuatavyo;
1. Kuongeza mapato ya ndani IBARA (20)
Mapato ya ndani yaliyokusanywa ni shilingi 12,767,482,352
ambayo ni sawa na 75.7 ya lengo la shilingi 16,830,702,000 kwa
mchanganuo ufuatao;
Kilolo DC 2,180,060,181, Iringa MC
3,526,582,802.93, Mufindi DC 2,837,351,416, Mafinga TC 1,580,742,133, Iringa DC
2,642,745,819
(e) ii Uhamasishaji umefanyika na jumla ya kaya
52,507 zimejiunga na mfuko wa afya ya jamii kwa mchanganuo ufuatao;
Iringa MC 9,385, Iringa DC
19,929,Mufindi DC 9,491, Mafinga TC 2,090, Kilolo DC 11,612
2.
Kilimo na Ushirika IBARA (22)
(a) Kuongeza
upatikanaji wa pembejeo na kusimamia matumizi ya pembejeo za ruzuku kwa kaya
Halmashauri zote zilipokea pembejeo na
kusimamia ugawaji wa pembejeo kwa kutumia mfumo wa vocha ambapo jumla ya vocha
228,000 zimetolewa kwa kaya 76,000 kwa
mchanganuo ufuatao; Iringa MC vocha
13,680 kwa kaya 4,560, Iringa DC
vocha 75,240, kwa kaya 25,080, Kilolo DC vocha 57,000 kwa kaya
19,000,Mafinga
TC vocha 22,800 kaya 7,600 na Mufindi DC
vocha 59,280 kwa kaya 19,760
(d)ii Kuwezesha vikundi 15
vya Wakulima kuzalisha mbegu za kuazimia ubora (QDS).
Jumla ya vikundi 9 vya Wakulima wa
kuzalisha mbegu za kuazimia ubora (QDS) vimewezeshwa kwa mchanganuo ufuatao;
Kilolo DC 4 na Mafinga TC vikundi 4 na Mufindi DC 1
(d)iv
Kuimarisha vikundi vya vijana kwa kuvipatia mafunzo.
Jumla ya wakulima 359 wamepatiwa mafunzo ya
viuagugu katika Kilimo ambapo kati yao vijana 224 na wanawake 135 kwa
mchanganuo ufuatao;
Manispaa -wanawake 97 na vijana 49, Kilolo
DC- vijana 127 na wanawake 18 Mafinga TC-
Vijana 48 na Wanawake 20.
(g)i
Kujenga masoko 2 na maghala 5.
Maghala 2 ya
kuhifadhia mazao katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa yanaendelea kujengwa
ambapo hali ya ujenzi imefikia asilimia 45
3.
Mifugo (IBARA25)
(e) Kuanzisha
mashamba darasa 18 ya malisho.
Jumla ya
mashamba darasa 15
ya malisho yameanzishwa ili wafugaji wa asili wajifunze jinsi ya kuboresha na kuhifadhi
malisho (feed banks) hususan wakati wa kiangazi na ukame kwa mchanganuo
ufuatao; Iringa MC 1, Iringa DC 7, Mufindi 4 na Kilolo 3
(g) Kutoa elimu kwa wafugaji.
Elimu imetolewa kwa wafugaji 253
kwa mchanganuo ufuatao Iringa DC 93, Kilolo DC 54,
Mufindi DC 71 na Mafinga TC 36
4. UVUVI (IBARA 27)
(K) kuiendeleza Sekta ya Uvuvi
Jumla ya vikundi vitano (5) vya vijana (3) na wanawake (2) vya ufugaji wa samaki vimeanzishwa
katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Halmashauri nyingine zinaendelea na uhamasishaji.
(L) Ujenzi mabwawa ya samaki
Jumla ya mabwawa ya samaki 20 yamejengwa
kwa kushirikiana na wadau wa ufugaji
samaki ili kuongeza uzalishaji wa samaki kwa mchanganuo ufuatao; Iringa MC 1,
Mafinga TC 2,Iringa DC 17
5. Utalii (IBARA 29)
(e) Kuongeza idadi ya wananchi wanaotembeela
vivutio vya utalii.
Jumla
ya Wananchi 1300 wametembelea vivutio vya utalii kwa mchanganuo ufuatao; Iringa
MC 410, Iringa DC 210, Kilolo DC
320 na Mufindi DC 360
6. Sekta ya Maliasili(IBARA 29)
(d)ii Kuongeza idadi ya mizinga ya kisasa ya
nyuki
Jumla ya mizinga 17,715 ya kisasa ya nyuki
imeongeka kwa mchanganuo ufuatao; Iringa MC 205, Mufindi DC- 5717, Kilolo DC
7790 na Iringa DC 4,003.
(f)
Kuongeza eneo la kupanda
miti.
Jumla ya hekta 11,792.65 za eneo la kupanda
miti limeongezeka kwa mchanganuo ufuatao; Iringa MC hekta 200, Kilolo DC hekta
11,213, Iringa DC hekta 12 na
Mafinga TC hekta 367.6.
7. Sekta ya Ardhi (IBARA 37).
(a)iv Kuongeza upimaji wa viwanja.
Jumla ya viwanja 494 na mashamba 3,778
yamepimwa kwa mchanganuo ufuatao;
Iringa
MC viwanja 183, Mufindi DC Mashamba 2124, Kilolo DC Mashamba 475,
Mafinga TC viwanja 300 na Iringa DC viwanja 11 na mashamba 1,179.
(a)viii
Kutoa elimu kwa Vijiji 360 na Mitaa
222 juu ya Sheria za Ardhi na Sheria ya
Mipangomiji
Elimu imetolewa kwa Vijiji 19 na Mitaa 9
juu ya Sheria za Ardhi na Sheria ya Mipango miji kwa mchanganuo ufuatao; Iringa
MC Mitaa 5 , Mufindi DC Vijiji 8, Kilolo
DC Vijiji 5 Mafinga TC-Mitaa 4 na Iringa DC Vijiji 6.
(a)ix Kuanzisha
na kuyaendeleza mabaraza ya ardhi
Jumla ya Mabaraza ya Ardhi 52 yameundwa ili
kufanikisha suala la utatuzi wa migogoro ya ardhi kwa mchanganuo ufuatao;
Iringa MC 18, Mufindi 4, Kilolo DC 23, Mafinga TC
5 na Iringa
DC 2
8.
Utayarishaji wa Mipango ya Matumizi Bora ya ardhi nchini (IBARA 37 B)
(b)iv
Kuongeza kasi ya utoaji wa Hatimiliki za Kimila
Jumla ya hati miliki za kimila 3,926
zimetolewa kwa Wananchi kwa mchanganuo ufuatao; Mufindi DC 1,882, Kilolo DC 865
na Iringa DC 1,179
(b)v
kuongeza kasi ya utoaji wa Hatimiliki
Jumla ya hatimiliki 1460 zimetolewa kwa
mchanganuo ufuatao;Iringa MC 1020, Mufindi DC 14, Kilolo DC 67, Mafinga TC 304 na Iringa DC 55
9.
Nyumba (IBARA 37 (C))
(b)ix Kuelimisha na kuhamasisha wananchi kujenga nyumba bora
Elimu imetolewa kwa Vijiji
8 na Mitaa 36 juu ya ujenzi wa nyumba bora kwa mchanganuo ufuatao; Iringa MC
Mitaa 20, Mufindi DC Vijiji 3, Kilolo DC- Vijiji 5 , Mafinga TC- mitaa 16
10.
USAFIRISHAJI NA UCHUKUZI (IBARA 39)
(b)ii Kujenga
barabara za lami na changarawe
Jumla ya
km 28.06 za kiwango cha lami
na km 285.5 za kiwango cha
changarawe zimetengenezwa kwa mchanganuo ufuatao; Iringa MC ( lami km 4.09 na
changarawe 2.5), Mufindi DC (lami Km
14.973 na changarawe Km 98) ,Kilolo DC (lami km 1 na changarawe km.156) Mafinga TC changarawe km
23 , Iringa
DC (Lami km 8 na changarawe km 29)
11.
AFYA (IBARA 49)
(a)
(i) Jumla ya Hospitali mbili (2), zahanati (21) na vituo vya afya
(6) vinaendelea kujengwa kwa mchanganuo ufuatao ; Iringa MC Hospitali (1),
Kilolo DC Hospitali (1), Vituo vya afya (5) na Zahanati (14). Mafinga TC
Zanahati (4 ), Iringa DC kituo cha afya
kimoja (1) na Zahanati(3)
12.
AFYA (IBARA 50)
(b)i Jumla ya
vyandarua 420,545 vimegawiwa kwa Wananchi kwa mchanganuo ufuatao; Iringa MC
42,589, Mufindi DC 146,634, Mafinga TC
44,556
na Iringa DC 186,766
(b)v Usambazaji wa
dawa umefanyika katika vituo 159 kwa mchanganuo ufuatao;
Iringa MC 21, Mufindi DC 62, Iringa DC 76
(P)
Jumla ya wazee 17,625 wametambuliwa na
kupewa matibabu bure kwa mchanganuo ufuatao; ; Iringa MC 1386, Mufindi
DC 14,558, Kilolo DC 200 na Iringa
DC
1,481
(q)v
vituo 105 vimepelekewa Dawa za kupunguza makali ya VVU na vifaa tiba kwa
mchanganuo ufuatao; Iringa MC 16 , Mufindi DC 22 na Iringa DC 67
13.
HUDUMA ZA JAMII (IBARA 52)
(a)i
Elimu ya awali
Jumla ya watoto 33,708 wa elimu ya awali
wameandikishwa kati ya lengo la kuandikisha watoto 28,712
kwa mchanganuo ufuatao; Iringa MC 3,283, Mufindi DC 9,740, Kilolo DC 8,390,
Mafinga TC 1,546 , Iringa
DC 10,749
(a)i Kuongeza idadi ya
madawati
Jumla ya madawati 24,533 yametengenezwa
kati ya lengo la kutengeneza madawati 29,347 Madawati hayo yametengenezwa
kwa mchanganuo ufuatao; Shule za Msingi
Madawati 21,304 na Shule za Sekondari
Madawati 3229,
(a)iii
kuhakikisha wanafunzi wote waliofaulu mtihani wa darasa la VII wanaendelea na
kidato cha kwanza kwa 100%.
Wastani wa 94.5% wa
wanafunzi waliofaulu mtihani wa darasa la VII
wamendelea na kidato cha kwanza kama ifuatavyo; Iringa MC 99.02%,
Mufindi DC 98%, Kilolo DC 92%, Iringa DC 89.2% .
(d)vi Kuendela kujenga
matundu ya vyoo kwa ajili ya wanafunzi wa shule za Sekondari.
Jumla ya matundu ya vyoo 96 yamejengwa katika shule za sekondari kwa mchanganuo
ufuatao;
Iringa MC 8, Kilolo DC 40, Iringa
DC 48.
(d)viii Kuendelea
kusimamia na kuimarisha michezo shuleni
Mashindano ya yanayohusisha shule za
Sekondari (UMISSETA) yamefanyia katika ngazi ya Wilaya na Mkoa.
14. Maji (IBARA 54)
(a)Kuboresha
huduma ya Maji Vijijini
Upatikanaji wa huduma ya maji safi na
salama umefika asilimia 71.2 na utekelezaji wa miradi yote ya maji ni kama
ifuatavyo;Iringa MC upo phase ya kwanza, Mufindi DC umefikia 30%. Iringa DC Mradi wa Maji Kikombwe na Weru umefikia 95%, Mradi wa Maji Mfyome
umefikia 80%, Mradi wa Maji Malinzinga umefikia 60%
(b)i Kuboresha huduma ya Maji Mijini.
Uboreshaji na upanuzi wa mitandao ya maji
eneo la makao makuu ya Mkoa umefikia asilimia 97.
(b)Viii Kuongeza
kasi ya ujenzi wa miundombinu ya utoaji wa majitaka
Halmashauri ya Manispaa inaendelea na kazi
ya ujenzi na ugawaji wa wateja kwenye mfumo wa majitaka kazi hii inafanywa na taasisi ya IRUWASA
ambapo imefikia 16.5%.
15.
UWEZESHAJI WA WANANCHI KIUCHUMI (IBARA 57)
(b)Jumla ya vikundi
vya ujasiliamali na VICOBA 873 katika
Mitaa 26 na vijiji 41 vimetambuliwa na kusajiliwa kwa mchanganuo
ufuatao; Iringa MC 741 katika Mitaa 20,
Mufindi DC 83 katika Vijiji 17, Mafinga TC-
vikundi 132 katika Mitaa 6, Iringa DC vikundi 49 katika vijiji 24.
(b)ii
Kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake na
vijana
Jumla ya vikundi 152 vya wanawake na vijana vimepatiwa mikopo kwa
mchanganuo ufuatao;Iringa MC Wanawake 6
vijana 4, Mufindi DC wanawake 28 vijana
28, Mafinga TC wanawake 5, Iringa DC wanawake 41 vijana 40.
(b)iii
Kutoa mafunzo ya ujasiliamali kwa vikundi
vya wanawake 170, vikundi 45
vijana
Jumla mafunzo ya ujasiliamali yametolewa kwa vikundi 243 kama ifuatavyo;
Iringa MC-Jumla ya vikundi 17, Mufindi DC wanawake 73 na vijana 17, Mafinga TC wanawake 15 na vijana 6, Iringa DC wanawake
81 na vijana 34
16.
KUENDELEZA MAKUNDI MAALUMU (IBARA 165)
Kuwatambua
wazee na kuwapa huduma ya matibabu katika vijiji ,mitaa na vitongoji.
Jumla ya wazee 17,625
wametambuliwa na kupewa matibabu bure kwa mchanganuo ufuatao; Iringa MC 1386,
Mufindi DC 14,558, Kilolo DC 200 na Iringa
DC
1,481
17.
WALEMAVU (IBARA 166)
Kuendelea
Kuwatambua na kuwalinda walemavu wote wakiwemo wenye elemavu wa ngozi katika
vijiji,mitaa na Vitongoji.
Jumla ya walemavu 151 wametambuliwa na kulindwa
kwa mchanganuo ufuatao; Iringa MC 22, Mufindi DC 81 na Mafinga TC 48.
18.
WANAWAKE (IBARA 167)
Kuhamasisha
wanawake kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika ngazi zote
katika vijiji
Elimu kwa wanawake ya kugombea nafasi
mbalimbali za uongozi katika ngazi zote
imetolewa katika Mitaa 49 na
vijiji 41 kwa mchanganuo ufuatao; Iringa MC Mitaa 38, Mufindi DC vijiji 20,
Kilolo DC vijiji 10, MafingaTC Mitaa 6 na Iringa DC vijiji 11
19.
WATOTO (IBARA 169)
Kuendelea
kutoa elimu juu ya sheria ya mtoto ya
mwaka ya 2009
Elimu juu ya sheria ya mtoto ya mwaka 2009 imetolewa kama
ifuatavyo; Mafinga TC Mitaa 5, Mufindi DC kata 19.
20.
VIJANA (IBARA 171)
Kufanya
uraghibishi wa vijana ili waweze kujiari katika nyanja mbalimbali kama kilimo,
ufugaji, ufundi sanaa
Uraghibishi wa Vijana katika nyanja mbalimbali kama kilimo,
ufugaji, ufundi sanaa umefanyika
katika Halmashauri zote kwa mchanganuo ufuatao;
Iringa MC Kata 10 Mufindi DC- Kata 3,
Mafinga TC kata 7, Iringa DC kata 5 kilolo DC kata 1.
CHANGAMOTO
KATIKA UTEKELEZAJI
Katika utekelezaji wa ilani kwa kipindi
husika Mkoa umeendelea kukabiliwa na changamoto kadhaa ambazo kwa namna moja au
nyingine zinafanya utekelezaji wake kutofanyika kama ilivyokusudiwa.
·
Uchakavu
wa magari ambao unasababisha kuongezeka kwa gharama za kuyahudumia pamoja na
uhaba wa vifaa vya kutendea kazi
·
Ufinyu
wa Bajeti kwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,Wakuu wa Wilaya na Halmashauri,
·
Ucheleweshaji
wa kutolewa kwa fedha na kutotolewa kwa fedha pungufu kwa ajili ya utekelezaji
wa miradi ya Maendeleo zilizoidhinishwa kutoka Hazina.
Mkoa, umejitahidi kuchukua hatua mbalimbali katika kukabiliana na changamoto hizo ikiwa ni
pamoja na;
·
Kuongeza
kiwango cha ukusanyaji wa mapato ya ndani katika Halmashauri ili kupata fedha
za kutosha kutekeleza miradi ya maendeleo kwenye Halmashauri husika.
·
Kuendelea
kufuatilia hazina fedha ambazo hazijatolewa ili ziweze kutolewa
·
Kuendelea
kuwashirikisha wadau mbalimbali chini ya mfumo wa PPP (Public Private
Partnership) katika kutekeleza shughuli mbalimbali.
TISHIO LA
KUANDAMANA NA UVUNJIFU WA AMANI
Kanuni
za Maadili ya Vyama vya Siasa zinatoa wajibu ambao
unavifanya
vyama vya siasa kuendesha shughuli zao kwa ustaarabu na uadilifu.
Ibara ya 5 ya Maadili hayo inaeleza kama
ifuatavyo;
5.–(1)Kila
chama cha siasa kitakuwa na wajibu
wa maadili chini ya kanuni hizi kwa:-
· kuzieleza kwa wanachama wake ili kuongeza uadilifu
wa kisiasa ndani na nje ya chama cha siasa;
· kulaani, kuepukana kuchukua hatua zitakazofaa ili kuzuia au kuepusha vitendo vya vurugu,
uvunjaji wa amani au ukandamizaji wa aina yoyote ile;
· kutotoa maneno yoyote au maandishi ambayo ni ya
uongo kuhusu mtu yoyote au chama cha siasa chochote;
· kulaani na kupinga
· matumizi ya lugha ya matusi
Kwa
kuzingatia Sheria, kila chama cha siasa kinatakiwa kuwa uhuru kushirikiana na
chama cha siasa kingine katika kuwaletea maendeleo wananchi na sio kusababisha
vurugu ndani ya eneo Fulani.
Hivi
karibuni tumesikia matamko ya viongozi wa kisiasa wakiwataka wananchi
kuandamana nchi nzima tarehe 01/9/2016. Kwa mkoa wa Iringa, nawaomba wananchi
kuwapuuza viongozi hao. Tuepuke maandamano na badala yake tufanye kazi kwa
bidii. Huu si wakati wa maandamano katika
Mkoa wa Iringa.
Nawaomba
sana wananchi, tuendelee kushirikiana, tufanye kazi kwa bidii na tuachane na
wahitaji wa mitaji ya kisiasa kwa sasa.
Muda
wa kutafuta mtaji wa kisiasa ukifika, wataruhusiwa kufanya maandamano. Wakuu wa
Wilaya, Maafisa Tarafa, Watendaji wa Kata, vijiji simamieni suala la amani
katika maeneo yenu.
Sitaruhusu
watu kuandamana nataka wananchi wote tufanye kazi kwa bidii.
Mwisho
Mkoa unatoa shukrani za dhati kwa Serikali
Kuu, Serikali za Mitaa, wahisani mbalimbali, sekta binafsi, Wananchi pamoja na
mashirika yasiyo ya Kiserikali kwa ushirikiano mzuri waliotupatia kuwezesha
kukamilika kwa utekelezaji wa Ilani kipindi hiki.
|
0 comments:
Post a Comment