Kada Johnson Mgima wakati akiwa katika mchakato wa kura za maoni CCM Ludewa
Na MatukiodaimaBlog
.......................................................................................
MWENYEKITI
mstaafu wa umoja wa vijana wa kanisa la Anglikana nchini Bw
Johnson Mgimba azitaka taasisi za dini na viongozi wa taasisi hizo
na wale wa vyama vya upinzani kuacha kufanya kazi ya kuikosoa
serikali ya Rais Dr John Magufuli na badala yake kumuacha Rais
aendelee kuwaletea maendeleo watanzania .
Bw
Mgimba ambaye pia ni kada wa chama cha mapinduzi (CCM) na
alipata kuingia katika mchakato wa kura za maoni ubunge jimbo la
Ludewa katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana aliyasema hayo wakati
akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusiana na
tabia ya baadhi ya watu wakiwemo viongozi wa dini kuacha kufanya
kazi za kuhubiri amani wamejigeuza kuwa ni wakosoaji wa serikali
jambo ambalo si jema .
"
Hizi taasisi za dini na viongozi wa makanisa wanakiwa kuacha
kujishughulisha na masuala ya
kisiasa na badala yake zitumike kuhubiri amani na upendo.. inasikitisha
sana kuona viongozi wa dini wanaacha kuhubiri upendo na amani
wao wanageuka kuwa wanasiasa wa kupandikiza chuki na kuikosoa
serikali kazi ambayo si yao''.
Alisema
kiongozi wa kiroho anapohubiri siasa badala ya neno la Mungu ilihali
anaowaongoza wana itikadi mbalimbali inaweza kuleta tafsiri tofauti na
kuwakwaza wengine walio na itikati tofauti na kiongozi wao hata wakati
mwingine makanisa kujikuta yanaliingiza Taifa katika machafuko
badala ya amani .
"Hakuna mgogoro mgumu kuutatua kama ule unaotokana na imani za kidini na
watanzania wanapaswa kuwa makini na viongozi wa aina hiyo ili
kutovuruga amani ya nchi ambayo imejengwa kwa muda mrefu"
Kwani
alisema kuwa makanisa
na taasisi za kidini zisiharibu na kuiaibisha madhabahu za Mungu kwa
kuhubiri siasa na badala yake kuwaacha wanasiasa wafanye ya siasa
na wao wafanye kazi yao ya kuliombea Taifa na kumuombea Rais Dr
Magufuli azidi kuchapa kazi zaidi .
Pasipo
kutaja makanisa hayo wala majina ya viongozi wanaogeuza
makanisa ulingo wa siasa alisema hivi sasa imezuka tabia ya
baadhi ya wanasiasa kuwatumia viongozi wa dini kueneza chuki zao
dhidi ya serikali kupitia viongozi wachache wa dini ambao
wanashindwa kutimiza wajibu wao wa kiroho .
Alisema
kama makanisa yanataka kufanya siasa basi yabadili usajili wao na kuwa
vyama vya siasa ili kuweza kuifanya kazi ya siasa kwa uhuru na ufanisi
zaidi kuliko kuendelea kugeuza makanisa majukwaa ya siasa .
Hivyo
alisema wananchi wote wa Tanzania bila kujali itikadi zao za
vyama wanapaswa kuwapuuza viongozi wa dini wanaotumia makanisa
vibaya na badala yake kuzidi kumuunga mkono Rais Dkt. John Magufuli
kwa mabadiliko makubwa anayoyafanya nchini .
Alisema
hakukuwa na nidhamu ya kazi, watu walifanya mambo ya ovyo ovyo bila
kujali na ili kurudisha hali kama ilivyokuwa miaka ya nyuma inatakiwa
kuwa na mwenye matendo kama anavyofanya Dkt. Magufuli. kuwa kitendo cha kuwapa fursa vijana kwenye nafasi za uongozi ikiwemo ukuu
wa mkoa, ukuu wa wilaya, ukurugenzi wa wilaya na nafasi nyingine
serikalini.
Bw Mgimba
alisema kinachotakiwa ni kwa vijana walioteuliwa kwenye nafasi
mbalimbali wasimwangushe Rais na kuwatumikia wananchi kwa kuchangia
kuleta maendeleo ya kweli kwao bila kujali itikadi wala dini zao.
|
0 comments:
Post a Comment