Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter
Msigwa amesema amewasilisha barua kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Job Ndugai akitaka Naibu Spika aondolewe madarakani
kwa kukiuka kanuni za uendeshaji Bunge.
Akizungumza na waandishi wa habari Msigwa
amesema kwamba muswada wa fedha uliopitishwa na Bungen lililomalizika
ulipitishwa kinyume na taratibu.
''Muswada wa fedha wa mwaka 2016 wenye
namba 9 ulichapwa tarehe tarehe 03 Juni 2016 na kusomwa bungeni kwa mara
ya kwanza na kwa utaratibu wa bunge ukaenda kufanyiwa kazi na kamati ya
bajeti na katika katika majadiliano na wadau ikaonekana muswada huo
ulihitaji marekebisho makubwa hivyo serikali ilitakiwa kuleta jedwali la
marekebisho jambo ambalo halikufuatwa''- Amesema Msigwa.
Msigwa ameongeza kuwa ''Naibu Spika
amekiuka kanuni na namna muswada huu ulivyopitishwa hata wabunge wa CCM
wengi hawakukubaliana nao ila yeye akaupitisha''
''Kwa mantiki hii nimemwandikia barua Spika
wa Bunge kwa kutaka kumuondoa Naibu Spika Tulia Ackson Mwasasu kwa
kushindwa kusimamia kanuni za bunge wakati wa kupitisha sheria ya fedha
ya mwaka 2016'' amesema Msigwa.
Wabunge wa kambi ya upinzania katika bunge
la 11 mkutano wa 3 uliomalizika walisusia vikao kwa zaidi ya wiki 3
wakitoka nje baada ya kudai kwamba Naibu Spika Dkt. Tulia Mwansasu
anaendesha Bunge isivyo.
Hata hivyo Naibu Spika alisikika akisema
anaendesha Bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na kama wabunge hao
wanatatizo na uendeshaji wake wa bunge watumie kanuni na si kususia
vikao vya bunge.
0 comments:
Post a Comment