Wanafunzi wa shule ya Southern Highlands Mafinga wakiwa katika mahafali yao ya 14 Mwaka jana
Na MatukiodaimaBlog
MKURUNGENZI
mtendaji wa shule ya Southern
Highlands Mafinga mkoani Iringa Bi Mary Mungai amewapongeza walimu
na wafanyakazi wa shule hiyo kwa kuiwezesha shule hiyo kuendeleza
rekodi yake ya kufanya vizuri katika matokeo ya mtihani wa Darasa
la Saba kiwilaya ,kimkoa na hata Taifa kwa miaka zaidi ya 13 sasa.
Bi
Mungai alitoa pongezi hizo kwa walimu wakati akielezea mafanikio
ya shule hiyo leo kuwa kwa mwaka huu shule hiyo imeweza
kuongoza tena kiwilaya kwa kushika nafasi ya kwanza kati ya shule
171 zilizopo wilayani Mufindi na shule ya 7 kati ya shule 467 katika
mkoa wa Iringa na kitaifa kuwa shule ya 888 kati ya shule 16,096
Hata
hivyo alisema kuwa kwa mwaka jana shule hiyo ya Southern
Highlands Mafinga ilikuwa nafasi ya kwanza kiwillaya kati ya shule
167 na kimkoa ilikuwa ya 8 kati ya shule 458 na kitaifa ilikuwa
nafasi ya 353 kati ya shule 15,867 kuwa matokeo ya mwaka huu
yameonyesha ni kwa kiasi gani jinsi walimu wa shule hiyo
walivyoendelea kujituma zaidi katika ufundishaji .
Alisema kuwa matokeo hayo ya darasa la
saba katika shule hiyo yanaonyesha ni kwa kiasi gani walimu
wanavyoendelea kuifanya shuler hiyo kutoa elimu ubora na sio
bora elimu hivyo kuwafanya wazazi waliowengi kuendelea kuchagua
shule hiyo
kwa ajili ya kuwapatia elimu bora.
Mkurugenzi
huyo alisema siri kubwa ya walimu kufanya kazi vizuri inatokana
na ubunifu wa safu ya uongozi wa juu wa shule hiyo kwa kuwapa
motisha walimu kila mwaka pindi wanapofanya vizuri katika mitihani
na kwa wanafunzi pia wamekuwa wakipongezwa toka wanapoanza darasa
la awali hadi wanapomaliza pindi wanapofanya vizuri katika mitihani
yao.
Alisema kuwa shule ilianzishwa mwaka 1994 kama
chekechea kwa jina la Lusungu Day Care Center ,Mwaka 1997 ilikuwa
na kuanza shule ya msingi -primary school ndiyo sasa inaitwa
southern Highlands yenye usajili wake namba IR03/7/001 ya mwaka 1997
ambapo imekuwa ni shule ya pili kufunguliwa baada ya Brook Bond
“ Uongozi wa shule umekuwa ukihakikisha unakuwa na
mpango endelevu wa kuboresha mazingira ya shule pamoja na
kuboresha elimu zaidi ili shule hiyo kuendelea kubaki ya mfano
katika taalum mkoa wa Iringa na nje ya mkoa wa Iringa"
Aidha alisema kuwa mbalia ya wanafunzi
wa shule hiyo kuwa na utaratibu wa kufundishwa masomo mbali mbali
darasani ila bado shule imekuwa na utaratibu wa kuwapeleka
wanafunzi katika mafunzo maeneo mbali mbali yakiwemo ya vivutio vya
utalii katika Tanzania bara na visiwani lengo likiwa ni kukuza
uelewa zaidi wa watoto hao.
Bi Mungai alisema kuwa mbali
ya kutembelea maeneo mbali mbali ya nje ya mkoa pia shule imekuwa
na utaratibu wa kuwapeleka kujifunza pia katika mashirika yaliyomo
ndani ya mkoa wa Iringa na Njombe .
alisema
ushirikiano mzuri ambao wazazi wamekuwa wakionyesha katika shule
hiyo hivi sasa tayari shule hiyo imeanzisha shule ya
sekondari ambayo inawawezesha wanafunzi hao kuendelea na elimu
ya sekondari na kama njia ya kuondoa usumbufu wa wanafunzi kukosa
nafasi za sekondari pindi wanapofaulu .
Kwa upande wake kaimu afisa
elimu wa Nasibu A. Mengele alisema kuwa kati ya shule ambazo
zimekuwa zikiupatia sifa mkoa wa Iringa kwa kufanya vizuri katika
mitihani ya darasa la saba ni pamoja na shule hiyo ya Southern
Highlands Mafinga hivyo wao kama viongozi wa elimu wataendelea
kuitolea mfano shule hiyo kila sehemu na ikiwezekano kuitangaza zaidi
ili wazazi kusomesha watoto wao katika shule hiyo.
Mwalimu
mkuu wa shule hiyo Bw Joson Nyang'wara alisema kuwa jumla ya
wanafunzi 51 ndio waliofanya mtihani wa darasa la saba na
wanafunzi wote wamefaulu katika mtihani huo hivyo alisema kuwa
suala la wanafunzi hao kukosa nafasi halipo kwani tayari shule hiyo
ya Southern Highlands Mafinga imekwisha kamilisha shule yake ya
sekondari ambayo imeanza kazi toka mwaka jana.
0 comments:
Post a Comment