Home » » JIMBO LA IRINGA MJINI LILIKOSA MBUNGE MAKINI SASA NI ZAMU YANGU UBUNGE -MWAKALEBELA‏

JIMBO LA IRINGA MJINI LILIKOSA MBUNGE MAKINI SASA NI ZAMU YANGU UBUNGE -MWAKALEBELA‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mgombea   ubunge  jimbo la  Iringa mjini Frederick Mwakalebela  akiomba kura kwa  wananchi wa kata ya Mshindo  leo  wakati wa mkutano wake wa kampeni
Wananchi   wakiwa katika  mkutano  huo wa kampeni leo
Aliyekuwa  mgombea  ubunge  katika mchakato wa ndani ya  chama Michael Mlowe  akimnadi Mwakalebela
Katibu  wa CCM Iringa mjini Bw Elisha Mwampashi  akimnadi  Mwakalebela
Wana CCm na  wananchi wa kata ya  Mshindo   wakisukuma  gari alipopanga mgombea  ubunge wa CCM Bw  Mwakalebela na mgombea  udiwani wa kata  hiyo Bw Ibrahim Ngwada leo
Wanananchi  na  wana CCm wakisukuma gari la Mwakalebela
Na matukiodaima Blog
MGOMBEA Ubunge wa jimbo la Iringa kupitia chama cha mapinduzi ( CCM) Frederick Mwakalebela amesema jimbo la Iringa Mjini limekosa kunufaika na fursa za maendeleo kwa kuwa halikuwa na mbunge makini wa kuleta maendeleo .


Hivyo amewataka wananchi wa jimbo la Iringa Mjini kuecha kujutia kukosa maendeleo na badala yake kumchagua kuwa mbunge wao ifikapo Octoba 25 mwaka huu.

Mwakalebela ametoa kauli hiyo leo wakati wa mkutano wake wa kampeni za Ubunge kwenye kata ya Mshindo  alisema iwapo atachaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo atahakikisha anasogeza maendeleo ya haraka kwa wananchi wa Jimbo la Iringa ambao kwa miaka mitano wamekosa kupata maendeleo hayo .

Kwani alisema hakuna sababu ya kujutia na badala yake kutumia nafasi hiyo kujutia miaka mitano ambayo wamepumzika pasipo kushuhudia maendeleo yoyote katika jimbo hilo la Iringa mjini.

Kuhusu nini atafanya baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge alisema ni pamoja na kuboresha miundo mbinu ,kuanzisha saccos ya vijana ,kuanzisha mfuko wa elimu wa jimbo kwa kutumia sehemu ya mshahara wake ,kuwawezesha wazee kupata matibabu ya bure na kuboresha sekta ya michezo.


Wakati aliyekuwa Mgombea Ubunge katika mchakato wa kura za maoni Balozi Augustino Mahiga alisema matumaini mapya ya jimbo la Iringa yatapatikana kwa kuchagua diwani ,mbunge na Rais toka CCM .

Kwani alisema kuwa majuto ya wanajimbo la Iringa ambayo wanayo kwa sasa ni kutokana na kukosa mbunge Makini wa kuwatumikia wananchi na badala yake kuwa na mbunge wa maandamano na fujo bungeni.

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa