Home » » MCHUNGAJI MSIGWA UBUNGE IRINGA MJINI HAPATI TENA

MCHUNGAJI MSIGWA UBUNGE IRINGA MJINI HAPATI TENA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mgombea  ubunge  jimbo la Iringa mjini Bw Frederick  Mwakalebela  kushoto  akiwa ameongozana  na katibu wa CCM wilaya ya Iringa mjini Bw Elisha Mwampashi
Mwakalebela  kushoto akimnadi amgombea  udiwani wa kata ya Kwakilosa Bw Hamid Mbata
Na MatukiodaimaBlog
CHAMA  cha wazee  wilaya ya  Iringa mjini  kimesema  kuwa kutona na  mbunge aliyemaliza  muda  wake  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa (Chadema)  jimbo  hilo kwa  sasa wanatamani  kuona  linarudi kwa mgombea  wa chama  cha mapinduzi (CCM) Bw  Frederick Mwakalebela .

Katibu  wa  chama  hicho  cha  wazee  wilaya ya Iringa mjini  Edson  Sanga alisema    hayo  katika  viwanja  wa CCM wilaya ya  Iringa mjini kuwa jimbo  hilo la Iringa mjini  limeonekana  kuwa  nyuma  kimaendeleo  kutokana na mbunge  aliyekuwepo kuendekeza marumbano  zaidi na  serikali na  kushindwa kufanya kazi ya  kuwatumikia  wananchi wake kama  ilivyo kwa  wabunge  wengine wa CCM wanaomzunguka kama Isimani kwa  Bw  wiliam  Lukuvi na jimbo la Kalenga  kwa  Godfrey  Mgimwa .

Alisema kasi  ya  maendeleo  katika majimbo jirani  huwezi  linganisha na  jimbo la Iringa mjini ambalo maendeleo  yanayoonekana ni yale  aliyoacha  aliyekuwa mbunge wa  jimbo hilo Bi Monica Mbega  na  kipindi  cha miaka  mitano ya Mchungaji Msigwa katika  jimbo  hilo zaidi ya maandamano na   lugha  za kejeli  kwa  wananchi hakuna kilichofanyika ,hivyo  ni lazima wananchi  wa  jimbo la Iringa mjini kutorudia  kosa kama  la mwaka 2010

" Tunajua  wana CCM ndio  tuliompeleka  bungeni mchungaji Msigwa baada ya  chama ngazi ya  juu  kutosikiliza ma hitaji ya  wananchi wa  jimbo  hilo hasa  wana CCM ambao  walimpitisha katika  kura za maoni na  vikao  vya juu  kukata  jina lake ......ila kilichofanyika mwaka  huu kwa  kurejesha  jina la mshindi  huyo Bw Mwakalebela ni sawa na  kurejesha  ushindi  kwa CCM"

Bw  Sanga  alisema  yeye akiwa katibu wa chama cha  wazee  mwenyekiti  wake  alikuwa ni marehemu babake na Mwakalebela  na kuwa siku  zote wazee wa jimbo la  Iringa walikuwa kama wapweke  kutokana na mbunge huyo  kuendeleza makundi na  visasi .

 Alisema moja kati ya ahadi ambayo mchungaji Msigwa alipata  kuwaahidi  wazee  hao wakati wa kampeni ni pamoja na  kutenga bajeti kupitia mfuko wa  jimbo kwa ajili ya  kuwasaidia  wazee na yatima ila hadi  leo hajapata  kuonyesha hata  senti  moja iliyotengwa kwa ajili ya  wazee hao jambo ambalo linawafanya  kujutia kura  zao  walizompatia mwaka 2010.

Sanga  alisema  ilikuwa ni vema mbunge Msigwa angetembelea  kujifunza kwa mbunge wa mwaka mmoja wa jimbo la Kalenga  kijana Mgimwa ambae  ndani ya mwaka mmoja alifanya mambo makubwa  jimbo kwake  tofauti na  mbunge wa  miaka mitano ambae hana jipya la kuonyesha kwa muda  wote  aliokuwepo madarakani .

Huku  Bi  Salome Kalinga mkazi  wa Kihesa  Kilolo akidai  kuwa ushindi  wa CCM unatokana na wana CCM wenyewe  na ushindi wa Chadema kwa  jimbo la Iringa mjini utaletwa na  wana CCM iwapo  wataendeleza makundi kama mwaka 2010 kwani  kihalisia  idadi ya  wana CCM na  wale wa vyama  vya upinzani jimbo la Iringa mjini bado CCM wapo  wengi  zaidi  ila makundi na visasi  za kisiasa  ndivyo  vinavyopelekea  chama kupoteza  ushindi  wake .

Katibu  wa CCM kata ya  Miyomboni Kitanzini Bw  Rayson  Shayo  alisema  kuwa kata  yake  ambayo ndio kata  iliyopo katikati ya mji wa Iringa hadi  sasa  wanajutia kumchagua  Msigwa  kutokana na vurugu za mara kwa mara  ambazo chimbuko lake ni mbunge  huyo  ikiwemo  vurugu ya machinga kuruhusiwa na mbunge   huyo  kufanya kazi  katikati ya  barabara.
Share this article :

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa