Home » » WAZIRI PINDA : TUTAUNGANISHA NGUVU KWA MGOMBEA URAIS ATAKAYE TEULIWA NA CHAMA‏

WAZIRI PINDA : TUTAUNGANISHA NGUVU KWA MGOMBEA URAIS ATAKAYE TEULIWA NA CHAMA‏


Waziri  mkuu  Mizengo  Pinda  akiwahutubia  wananchi  wa  tarafa  ya  pawaga  leo
Wananchi  wa tarafa  ya  pawaga  Iringa  wakimsikiiza waziri  mkuu Bw  Pinda
Wananchi  wa  tarafa  ya Pawaga wakimshangilia  waziri  mkuu Pinda leo
Waziri  mkuu akiwapungia  mikono  wananchi  wa tarafa  ya  Pawaga  leo

 Na Matukiodaima Blog
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amewataka watanzania hasa wana chama wa Chatham cha mapinduzi ( CCM) kuwa na subira katika kumpata mwanachama atakayefaa kusimama kugombea urais kupitia CCM mwaka huu. Kuwa tayari wengi sana wamejitangaza wazi wazi na wengine wamejitangaza kimya kimya kutaka kugombea Urais na kuwa yote heri ila chama kina utaratibu wake. 

 " Itafika wakati ambao kila chama kitasema huyu ndie mtu wetu ambae atapambana na vyama vingine ...tunachosema sisi huyo atakayependekezwa ndie atakuwa mgombea wetu"alisema Waziri 

Pinda Waziri Pinda alitoa kauli hiyo leo wakati akiwahutubia wakazi wa tarafa ya Pawaga Baada ya kuzindua skimu ya umwagiliji itakayowanufaisha wakazi wa vijiji vitatu kikiwemo cha Magozi,Ilolompya na Mkombilenga uliogharimu zaidi ya Tsh bilioni 1.6 fedha kutoka kwa wahisani na serikali. 

Alisema kuwa utaratibu wa ndani ya chama anbacho wao ni watawala na wanaoendelea kuyafanya maendeleo yanaonekana watalazimika kumuunga mkono atakayeteuliwa na wale wote ambao hawajateuliwa watamuunga mkono atakayeteuliwa kwa makundi yote kuvunjwa na kuwa na Kundi moja pekee.

 kuwa baada ya mgombea wa chama tawala kupatikana jukumu kubwa ni kuwaomba wapenzi wao wote kumchagua huyo aliyeteuliwa na chama. Hivyo Waziri Pinda aliwataka wananchi kote nchini kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga Kura.

 Alisema kuwa zoezi hilo ambalo litawahusu wale wote wenye miaka kuanzia 18 na kuendelea linataraji kuanza mwezi huu katika Mkoa wa Njombe na kuwa kila kata zoezi hilo litadumu kwa muda wa wiki mbili ama tatu .

 " Nawaombeni kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na pia kuipigia kura katiba inayopendekezwa muda ukifika sisi tunaamini ni katiba bora ambayo imegusa makundi yote yakiwemo ya wafugaji na wakulima pamoja na makundi mengine" 

Kuwa wapo wapotoshaji ambao watafika na kuwadanganya juu ya katiba hiyo inayopendekezwa na wasiwasikilize

 Alisema kazi kubwa imefanyika katika kuandaa katiba hiyo inayopendekezwa mbali ya wao (UKAWA) kutoka nje wakati wa bunge hilo la katiba lakini wajumbe waliobaki walifanya kazi nzuri ya kuandaa katiba hiyo inayopendekezwa hivyo kuwaomba wananchi kuipigia kura.

Katika hatua nyingine Waziri mkuu Pinda amewataka wakulima wa mpunga Pawaga katika kuepuka na migogoro kati yao na wafugaji kuweka utaratibu wa kukusanya majani ya mpunga na kuyapeleka majumbani kwao ili wafugaji wapate kununua kuliko kuyaacha mashambani na kuwafanya wafugaji kuingiza mifugo Yao mashambani.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa