Home » » WANA CCM NA CHADEMA LUDEWA WAMCHANGIA FEDHA YA KUCHUA FOMU YA UBUNGE FILIKUNJOMBE‏

WANA CCM NA CHADEMA LUDEWA WAMCHANGIA FEDHA YA KUCHUA FOMU YA UBUNGE FILIKUNJOMBE‏


Baadhi ya   wana CCM na  Chadema   kutoka kata ya  Kilondo  waliofika  katika  sherehe za  miaka 38  ya  CCM zilizofanyika  kiwilaya kata ya  Kilondo
Boti iliyowabeba  wana CCM na Chadema kwenda  katika  sherehe za  miaka 38 ya  CCM Ludewa ikiwa na rangi ya  Chadema bendera  ya  CCM
Mbunge  Filikunjombe  akiwa amebebwa juu juu kupelekwa  meza kuu

 Mbunge  wa  Ludewa  Deo  Filikunjombe  akicheza  ngoma  sanjari na  wasanii wa kikundi cha sanaa kutoka Kyela  Mbeya  siku ya  sherehe za miaka 38 ya  CCM



Vijana  wa  Chadema na  CCM  wakiwa wamembeba  juu  juu mbenge wa  Ludewa  Deo Filikunjombe  alipowasili  katika  kijiji  cha Kilondo kwa ajili ya  sherehe za miaka 38 ya  kuzaliwa kwa  CCM kiwilaya kijijini hapo
Vijana  wa CCM na  Chadema  wakiwa  wamembeba mbunge Deo  Filikunjombe
Mbunge  Deo  Filikunjombe  akihotubia katika  sherehe za miaka 38 ya  CCM wilaya  kwa  wilaya   ya Ludewa
Mwenyekiti wa kijiji  cha  Nsele  Bw
Wazee  wa  kata ya  Kilondo Ludewa wakitoa  baraka  zao kwa mbunge  wa  jimbo la  Ludewa Deo Filikunjombe baada  ya kumkabidhi  fedha  waliyochanga  kiasi cha Tsh 100,000 kwa  ajili ya  kuchukua  fomu ya  kuwania ubunge mwaka  huu

Na matukiodaimaBlog
WANACHAMA  wa  chama cha  Demokrasia  na maendeleo (CHADEMA ) na vyama  mbali  mbali  vya  upinzani  kata  ya  Kilondo  wilaya  ya  Ludewa   waungana  na wanachama    wa chama  cha  mapinduzi (CCM)   wilayani hapo    mkoani  Njombe     katika  kusherehe   miaka 38 ya  kuzaliwa  kwa   CCM huku wakimchangishana   kiasi   cha  Tsh 100,000  mbunge  wa  jimbo  la  Ludewa  Bw  Deo  Filikunjombe  kwa  ajili ya  kuchukua   fomu ya  kugombea  tena  ubunge  mwaka huu  katika   jimbo   hilo .

Pamoja na   tukio la kuungana  kwa pamoja  kusherekea  miaka 38 ya  kuzaliwa kwa  CCM na  kumcghangia  fedha  hizo  mbunge wao  bado  vijana  wa vyama  vya  CCM na  Chadema   walilazimika kumbeba juu juu umbali wa mita 500 mbunge  Filikunjombe na  mkuu  wa  wilaya  ya  Ludewa  Juma Madaha   huku  wakiwaita ni  viongozi shujaa  wa  wilaya ya  Ludewa na Taifa  la  Tanzania kutokana na  kufika  eneo  kijiji  cha Nsele na  kujitolea  kujenga Zahanati.

Tukio  hilo la aina   yake katika  Demokrasia na  vyama  vingi   nchini  Tanzania   lilitokea  juzi( Februari 15) mwaka  huu wakati  wa wana  CCM katika  wilaya ya  Ludewa  walipofanya sherehe  hizo kiwilaya katika  kata   hiyo ya Kilondo kwa mara ya  kwanza toka chama   hicho  kilipoanzishwa .
Akisoma  risala  ya    wananchi  wa  kata   hiyo  ya Kilondo mzee Bernad  Mwandesile (75)wa  kijiji cha Nsele    aliyeambatana   wazee  wenzake 12 pamoja na  diwani  wa  kata  ya  Kilondo  Bw, Hilmary Mwakipokile.

walisema kuwa   wamelazimika kuwa  wa kwanza  kumchangia kiasi  hicho  cha  fedha  kutokana na kipimo cha  uongozi ambacho wamempima  ndani ya  jimbo  hilo la  Ludewa na jinsi anavyo watumikia   vema  watanzania  kwa  ujumla  bungeni na  kuwa ahsante  yao kwa kazi kubwa anayoifanya  ndani  ya  jimbo  hilo na  nje ya  jimbo la  Ludewa  wameona  ni  vema  wasimpoteze na  badala  yake  kumpa  nafasi  zaidi ya  kuwa  mbunge  wao.

  Leo  hapa  mbele  yako  tupo wazee  ambao  tumewawakilisha  vijana  na  wannchi   wote  wa kata  yetu ya Kilondo kusema  haya  na  kukukabidhi  rasmi  mchango  wetu  huu  wa Tsh 100,000  ili muda  ukifika  ukachukue  fomu tena ya  kugombea  ubunge……tunajua  kuwa   kiasi  hiki cha   fedha  ni kidogo na hakitoshi  kuchukulia  fomu  ila uwezo  wetu  umeishia  hapo tunaamini  kuwa  fedha  nyingine  nyingi utaongeza  mwenyewe lakini  leo pokea hiki kidogo toka  kwetu  “walisema   wazee  hao katika  risala  yao kwa  mbunge Filikunjombe.

Kuwa mbali ya  mchango  huo na imani  yao  kubwa ya  kutamani  jimbo  hilo  kuendelea  kuwa mikononi mwa  mbunge   huyo bado walikionya  chama cha  CCM na  viongozi  wake  wa  kitaifa  kuwa  mbali ya mbunge  huyo  kutokea CCM ila wanamtambua  kama  mbunge anayewafaa hata  kama angechukua fomu kwa  Chadema ama  chama  kingine  chochote cha siasa  au yeye  mwenyewe  bila ya  kusimama kwa chama  chochote  bado  wasingechagua mbunge mwingine zaidi yake  hivyo viongozi  wa juu wa CCM wanapofanya maamuzi yao ya nani asimame  kugombea Ludewa  pia wapime kwanza  kuona  wananchi wanataka nini na nani  kwa ajili  ya  kuendeleza  wilaya  ya  Ludewa badala kuamua bila kujiuliza.

“……Tumepata   kuwa na  wabunge  hadi  sasa toka  nchi  hii  ipate  uhuru  mbunge  Filikunjombe ni wa nane  kuongoza jimbo la  Ludewa  ila tuwe  wakweli mbele ya mwenyekiti  wa CCM wilaya ya  Ludewa Stanley Kolimba ambae  pia  nae  yumo katika orodha  ya  wabunge   walioongoza  jimbo la  Ludewa ….mbunge aliyefanya mambo makubwa kama  haya ya  kimaendeleo  zaidi ya Filikunjombe hayupo …kweli  tumempata anayecheka na  sisi  wakati  wa  furaha na kulia na  sisi  wana Ludewa  wakati wa  shida hatuna haja  ya  hao  wanaojipitisha kwa  kutaka  kutuvuruga mlango tunaufunga  kwa  kumwomba  Deo Filikunjombe kuchukua fomu  tena pia mbali  ya  jina  lako maarufu la jembe letu  wana  Ludewa  bado  tunaomba  kukubatiza upya  hapa  leo kuwa utaitwa “Msamaria mwema” kuanzia  leo hii ni  kutokana na  moyo  wako  wa  utoaji ”

Wazee hao waliowakilisha  wenzao ni pamoja Joseph  Mwembeleko,  Annastasia Lupangaro, Abel Mwakipokile, Stanlaus  Mwambeleko, ,Melenia  Kilongo, Emmanuel  Mwakipokile, Yordan  Mwafingulo,,Sailis Ipungu,Maria Ngailo ,Bernad Mwansesile na diwani  wa kata  hiyo  Hilmary Mwakipokile.

Awali  diwani  wa kata   hiyo ya  Kilondo Bw ,Hilmary Mwakipokile pamoja na  kuomba  radhi  kwa mbunge  Filikunjombe mbele ya  wananchi wake  kwa kutoshiriki katika  sherehe  kubwa   ya  uzinduzi  wa mradi  wa  umeme  REA kata ya  Kilondo uliozinduliwa katika kijiji  cha Kilondo wiki  moja  iliyopita kwa madai  ya  kuwepo  kikazi  nje ya  wilaya ya  Ludewa  bado alisema  wapo  baadhi ya wana CCM wamekuwa wakipeleka taarifa  zisizo sahihi kwa  mbunge  huyo kwa lengo la kumchafua  kwa  kudai hayupo pamoja na mbunge  jambo ambalo  si  kweli na  yeye hawezi kuwa  mwanachama mwingine  yeyote anayetaka  ubunge  zaidi ya Filikunjombe .

“Nataka  kukuhakikishia  mbunge nimepita  vijiji  vyangu  vyote na  kuitisha mikutano na  kukutana na  wazee na  kuomba  radhi kwa kutokuwepo siku ya uzinduzi wa mradi wa umeme kweli nipo  nyuma yako na  kuendelea  kuunga  mkono kwa nguvu  zote shughuli za kimaendeleo unazoendelea kuzifanya hapa  kata ya  Kilondo  ulipounga  mkono  ujenzi wa Zahanati ya  Kilondo  mimi pia  nimekuunga mkono kwa  kuchangia mifuko 8  ya  saruji “

Mwenyekiti  wa  CCM wilaya ya  Ludewa  Stanlye Kolimba  mbali ya  kumpongeza mbunge  Filikunjombe kwa kazi  nzuri ya  kukijenga  chama  katika  wilaya ya  Ludewa  bado  aliwatoa   hofu  wananchi  wa  Ludewa  kuwa lengo la CCM ni  kuwatumikia  wananchi kwa  kuwasogezea  miradi  ya  kimaendeleo   hivyo CCM hakitapuuza  matakwa ya  wananchi juu ya mbunge  wao   huyo.

Akiwashukuru  kwa  mchango  huo wa fedha  ya kuchukulia  fomu mbunge  Filikunjombe  alisema  kuwa amefarijika  zaidi kwa  moyo  wa  upendo  walionyesha  wananchi  hao  wa kata ya  kilondo na  kwa  kuwa  wamemtangulia  kumwomba kugombea  ubunge kabla ya  muda  kufika  na  yeye  kutangaza  popote kama atagombea tena ama hatagombea  ubunge kwa mara  ya  kwanza anawatangazia  kuwa bado anaupenda  ubunge hivyo  muda  ukifika atachukua  tena  fomu.

“Sijapata kutamka sehemu  yoyote kama nitagombea  tena  ubunge ila  leo wananchi  wa kata ya  Kilondo mmenipa moyo  sana maana  pale  vijana  waliponibeba  juu juu walianza  kuvutana wenyewe kwa  wenyewe  kwa  wale  wa Chadema  kuniomba  kuwa mheshimiwa  tunakupenda  sana tunaomba  CCM  wakikukata  jina  lako ugombee kwa  chama  chetu …… huku  wale  wa CCM  wakisema hakatwi mtu  wewe  wetu ila uamuzi  huu  wa wazee  kuamua kujichangisha na kunipa fedha  ya  kuchukua  fomu ….kweli  sitapata  kutangaza  popote na muda  bado wa kufanya   hivyo ila nasema kwa  moyo na upendo huu mlionipa leo nasema nitagombea tena  ubunge “

Mbunge  Filikunjombe  alisema  mbali ya  kuwa  sherehe   hizo ni za CCM  ila ameshangazwa sana na  kuvutiwa na  wananchi  wote wa kata   hiyo kuacha  shughuli  zao na kufika kumpokea na  kusherekea miaka 38 ya  CCM jambo ambalo ni kielelezo tosha  kuwa wanampenda .

Alisema  katika  kusogeza maendeleo kata  hiyo ya  Kilondo amelazimika kujitolea  kujenga  zahanati  ya  kijiji  cha Nsele  pamoja na  kukabidhi  vifaa mbali mbali kama  magodoro 25 kwa  Zahanati ya  Kilondo ambayo  wagonjwa  walikuwa  wakilala chini , Sementi, mifuko 150,bati za  kutosha  zahanati  inayojengwa  na  kulipia mafundi  wanaojenga  zahanati hiyo  na  kufanya  jumla ya thamani ya msaada  wote  kufikia  zaidi ya Tsh milioni 13.

Kwa  upande  wake  mkuu wa  wilaya ya Ludewa Juma Madaha pamoja na  kumpongeza  mbunge  huyo kwa  kuwasaidia  wananchi hao ujenzi  wa Zahanati  pia  aliahidi  kumuunga mkono kwa  kuchangia kiasi  cha Tsh 500,000.
MWISHO
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa