Home » » WANAWAKE KITELEWASI VINARA KUJIFUNGULIA MAJUMBANI

WANAWAKE KITELEWASI VINARA KUJIFUNGULIA MAJUMBANI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
WANAWAKE wa Kijiji cha Kitelewasi Kata ya Rungemba Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa, wanaongoza kwa kujifungulia majumbani licha ya elimu kutolewa kuhusu umuhimu wa kujifungulia katika vituo vya afya na zahanati.
Akizungumza na Tanzania Daima, muuguzi wa zahanati ya Rungemba, Suzan Mhngole, alisema pamoja na kujitahidi kutoa elimu kijiji hadi kijiji, bado suala la kujifungulia katika zahanati, vituo vya afya na hospitali kwa wananchi wa Kitelewasi ni changamoto.
Mhongole, alisema asilimia kubwa ya wanawake wanaobeba mimba katika kijiji hicho ni wabishi wa kufuata maelekezo na ushauri wa wataalam pindi wanapofika kliniki, na mwishoni hujifungulia majumbani mwao bila kujali matatizo yanayoweza kujitokeza.
Alitaja sababu za kujifungulia majumbani ni kuwa, wengi wanapopewa rufaa ya kwenda kujifungulia hospitali ya Wilaya, wamekuwa hawafanyi hivyo na badala yake huenda kujifungulia majumbani.
“Tunapogundua kuwa mjamzito ana vidokezo vya hatari, tunamuandikia rufaa ya kwenda katika hospitali kubwa lakini wengi tunaowaandikia rufaa… wamekuwa hawaendi na badala yake wanaamua kwenda kujifungulia majumbani mwao,” alisema.
Kata ya Rungemba ina vijiji vitatu, ambavyo vyenye zahanati ni Rungemba na Itimbo huku Kitelewasi ikiwa haijakamilika kujengwa.
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa