Home » » MSECHU AWAPA SOMO WAKINGA

MSECHU AWAPA SOMO WAKINGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
WENYEJI wa Makete mkoani Njombe wanaoishi sehemu mbalimbali nchini, wamekumbushwa wajibu waliyonao katika kuiendeleza Wilaya hiyo ili ikue kiuchumi.
Wito huo ulitolewa hivi karibuni na Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba Tanzania (NHC), Nehemia Msechu, alipofanya ziara ya kikazi wilayani humo kwa lengo la kutembelea eneo litakalojengwa nyumba za bei nafuu kwa wakazi wa Makete.
Alisema kabila la Wakinga ni wawekezaji wakubwa katika miji mbalimbali, lakini inashangaza kuona wanasahau kuiendeleza Wilaya wanayotoka na wangewekeza ingekuwa ni moja ya Wilaya yenye nguvu nchini Tanzania.
“Inashangaza kuona Wilaya hii yenye hali ya hewa nzuri ikiwa katika hali hii… ili hali tunashuhudia wazawa wa Wilaya hii wakifanya mambo makubwa jijini Dar es Salaam hasa maeneo ya Kariakoo na sehemu mbalimbali nchini,” alisema Msechu.
Alitoa wito kwa wazazi, uongozi wa Wilaya, viongozi wa dini na wadau wengine wa maendeleo wilayani hapa, kuendelea kuwashawishi ili warudi nyumbani na kuwekeza.
Taarifa kutoka jijini Dar es Salaam, zinaonyesha wakinga kwa kupitia umoja wao, wamekuwa wakinunua nyumba za wenyeji na kujenga nyumba nyingi za ghorofa kama vitega uchumi vyao.
Mbali na Dar es Salaam, Wakinga wanaonyesha uwezo wao kifedha katika maeneo mikoa kama Morogoro, Arusha, Mwanza, Dodoma, Iringa na Mbeya.
Chanzo; Tanzania Daima 

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa