Home » » JUMUIYA YA WATUMIAJI MAJI NZIHI WAPATIWA PIKIPIKI

JUMUIYA YA WATUMIAJI MAJI NZIHI WAPATIWA PIKIPIKI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
MKURUGENZI wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wa Kampuni ya Simu Tigo, Jackson Kiswaga ametoa msaada wa pikipiki kwa jumuiya ya Watumiaji Maji Kata ya Nzihi kwa lengo la kumaliza kero iliyokuwa inawakabili ya usafiri ili kuwawezesha kutembelea mitambo mbalimbali kwa urahisi.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo yaliyofanyika hivi karibuni katika ofisi za kata hiyo, Kiswaga aliahidi kuendelea kushirikiana na wananchi katika kuwaletea maendeleo.
Alisema apatapo fursa ya kukutana na watu wa ndani na nje ya nchi wanaoweza kusaidia maendeleo ya watu wengine amekuwa akiyakumbuka matatizo ya wananchi wa Iringa na kuomba msaada.
“Hakika katika kuleta maendeleo nitahakikisha nashirikiana na wenzangu katika maendeleo yetu, sitaacha kutoa mchango wangu, nimefanya hivyo muda mrefu uliopita, nafanya hivi sasa na nitaendelea kwa siku zijazo,  nimekutana na wadau kutoka Marekani, Ulaya na Afrika Kusini kuna mambo yanakuja katika sekta ya afya na elimu na yatakapokuwa tayari nitawaleta ,”  alisema Kiswaga.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Steven Mhapa ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Nzihi, alisema chombo hicho cha usafiri kitaiwezesha jumuiya hiyo kusafiri eneo moja hadi lingine kufuatilia maendeleo na changamoto zinazoukabili mradi huo wa maji.
Naye Meneja wa Watumiaji Maji Kata hiyo, Hamza Chorobi, alisema mradi huo wa maji una changamoto kama vile uchakavu wa miundombinu yake na ongezeko la watumiaji wa huduma hiyo, hivyo unahitaji zaidi ya sh milioni 300 kwa ajili ya ukarabati.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa