Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MAMLAKA ya majisafi na majitaka Manispaa ya Iringa (Iruwasa),
imewaasa wananchi kuwa makini na uunganishaji maji kinyemela kwenye
mtandao wa huduma hiyo kuepuka usumbufu na sheria kali
zitakazochukuliwa dhidi ya watakaobainika.
Msimamizi Mkuu Kitengo cha majitaka na usafi wa mazingira Iruwasa,
Yohana Bugando, alisema kumekuwa na ongezeko la wananchi
wanaounganishiwa huduma ya majisafi na taka kwa kutumia mabomba ‘feki’
na mafundi ambao hujitambulisha wametumwa na mamlaka hiyo kumbe ni
‘vishoka’.
Bugando, aliongeza kuwa hali hiyo husababisha kupotea kwa maji
kutokana na mabomba kupasuka na kuvuja mitaani kutokana na kutokuwa
imara.
Aliwaasa wananchi kufuata utaratibu wa kuunganishiwa huduma ya maji
kwa kutuma maombi kwa uongozi wa serikali za mitaa, maofisa ardhi wa
eneo husika na hatimaye Iruwasa ndiyo yenye mamlaka ya kutoa huduma ya
uunganishaji wa mtandao wa maji safi na taka.
Aliongeza kuwa, Iruwasa inaendelea na mpango wa kuhakikisha wakazi wa
Kata za Ilala, Makorongoni, Mivinjeni na Gangilonga Manispaa ya
Iringa, wanaunganishwa na huduma ya maji taka hivyo wananchi waepuke
kutupa vitu vigumu na mchanga kwenye mabomba ya maji taka.
Chanzo:Tanzani Daima
0 comments:
Post a Comment