Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MABASI ya abiria ‘daladala’ yanayofanya safari zake mjini Iringa,
jana yaligoma kwa saa 8 na kusababisha usumbufu kwa wakazi wa Manispaa
ya Iringa na viunga vyake.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti madereva wa daladala hizo walisema
sababu ya mgomo ni baadhi ya bajaji kuchukua abiria mithili ya daladala
na kuwakosesha mapato.
Dereva Moses Job alisema bajaji zinafanyakazi za daladala huku
mamlaka ya usafirishaji ikishindwa kuwachukulia hatua na kusababisha
mgomo huo.
Mgomo huo ulimlazimu mwandishi wa habari hii kwenda ofisini kwa Mkuu
wa Kikosi cha Usalama barabarani, Leopord Fungu na kushindwa kumwona
baada ya kuambiwa yupo katika kikao na viongozi wa Kamati ya Usalama
barabarani ya mkoa.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment