Home » » KUSANYENI KODI ZA MAJENGO-WAZIRI NCHEMBA

KUSANYENI KODI ZA MAJENGO-WAZIRI NCHEMBA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amezitaka halmashauri za wilaya, miji, manispaa na majiji kuongeza mapato kwa kukusanya kodi za majengo badala ya kukimbizana na wafanyabiashara ndogondogo na wajane.
Akizungumza na wananchi wa Manispaa ya Iringa kwenye Uwanja wa Mwembetogwa baada ya kumsimika Salim Abri kuwa kamanda wa Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa wa Iringa, Nchemba alisema tabia ya halmashauri na Serikali kushughulika na wafanyabiashara wadogo na kuwaacha wakubwa wakiendelea kukwepa kodi, imepitwa na wakati.
“Naziagiza halmashauri nchini kuacha kukimbizana na wajane wanaouza matembele (mboga za majani) na samaki wachache, badala yake wakusanye kodi za majengo ambazo ni nyingi,” alisema.
Alisema duniani kote utaratibu ni kukusanya kodi kubwa kwa matajiri ili kutoa huduma bora kwa maskini kwa kuwaboreshea huduma mbalimbali.
Alisema kinachotakiwa ni kuwafichua wote wenye majengo wanaokwepa kulipa kodi, jambo ambalo linawezekana kufanikiwa zaidi kwa kuwapata viongozi bora kupitia Serikali za mitaa.
Vilevile alisema mpango wa Serikali hivi sasa ni kupunguza matumizi na kuongeza mapato, ambapo wameanza na elimu kwa kulipa mishahara kupitia kwenye akaunti za walimu moja kwa moja ili kudhibiti mishahara hewa.
Aliwataka watumishi waliokuwa wanafuja fedha za umma kupitia mishahara hewa watafute kazi kwingine, kwani mwisho wao umewadia.
Aliwaonya watumishi wa umma kuacha matumizi mabaya ya fedha za wananchi ilihali walipa kodi wakiwa na matatizo mengi yanayohitaji kutatuliwa.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa