Home » » WANANCHI WAHIMIZWA KUPANDA MITI

WANANCHI WAHIMIZWA KUPANDA MITI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MKUU wa Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa, Evarista Kalalu, amewataka wananchi  wa wilaya hiyo kujenga tabia ya kupanda miti na kutunza mazingira kwa lengo la kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabia nchi yanayoendelea duniani kote.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Vikundi vya Kijamii Mufindi (Uvikimu) unaojihusisha na uoteshaji wa miche ya mbao na matunda, ufugaji wa nyuki, pamoja na ufugaji wa kuku, Kalalu alisema upungufu wa mvua kwa baadhi ya maeneo ni matokeo ya kudharau ushauri huo ambao hutolewa kila mara kwa wananchi.
Kalalu alipongeza hatua ya Uvikimu na kusema ni hatua muhimu kwa wanajamii wote kutambua umuhimu wa kuhifadhi mazingira, ili kuendelea kunusuru maisha ya viumbe hai na mmomonyoko wa udongo.
Ofisa Maendeleo ya Vijana Wilaya ya Mufindi, Juma Fuluge, alisema uelewa mdogo wa wananchi kushindwa kujiunga na vikundi mbalimbali vya ujasiriamali ni jambo linalorudisha nyuma  maendeleo, hivyo kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi  kujiunga katika vikundi hivyo, ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Baadhi ya wajasiriamali  wameendelea kulia na ukosefu wa mitaji na masoko ya kuuzia bidhaa zao na kuomba serikali kuwaangalia kwa jicho la huruma.
Uvikimu imeanzishwa mwaka juzi na hadi sasa ina wanachama 770 kutoka katika vikundi 35.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa