Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Majalada mawili yaliyofunguliwa na polisi katika sakata la
kutekwa kwa Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Rose Kamili yamefikishwa
kwa Mwanasheria wa Serikali kwa ajili ya hatua zaidi.
Kamili alituhumiwa kutoa rushwa kwa wananchi wa
Kijiji cha Kitayawa, Kata ya Luhota wakati wa uchaguzi mdogo wa Jimbo la
Kalenga.
Jalada la kwanza ni la tuhuma za kutoa rushwa
zinazomkabili mbunge ambazo zilitokana na walinzi wa CCM kumkamata
wakidai alikuwa akifanya uhalifu huo na pili linahusu madai ya Kamili
kuwa alitekwa, kudhalilishwa na kupigwa na wana-CCm hao.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Wankyo
Nyigesa alisema jana kuwa uchunguzi wa polisi umekamilika na
wameyafikisha majalada hayo kwa Mwanasheria wa Serikali kwa ajili ya
hatua zaidi.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment