Home » » WAJASIRIA MALI 700 IRINGA WAPATIWA MAFUNZO

WAJASIRIA MALI 700 IRINGA WAPATIWA MAFUNZO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
ZAIDI ya wajasiriamali 700 waliopatiwa mafunzo ya kutengeneza batiki, sabuni na keki wametakiwa kutumia elimu hiyo kwa vitendo ili wajikwamue kimaisha na kuongeza pato la taifa.
Wito huo umetolewa juzi na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mjasiriamali Kwanza ya jijini Dar es Salaam inayoendesha mafunzo hayo, Dk. Didas Lunyungu, katika semina iliyowahusisha wajasiriamali zaidi ya 700 wa Mkoa wa Iringa.
Dk. Lunyungu alisema lengo la semina kwa wajasirimali hao ni kuwajengea uwezo wa kujitegemea kupitia kazi za mikono na malighafi zinazowazunguka ili wainue  vipato vyao na taifa.
“Hapa mna rasilimali za kutosha, hamuwezi kujikwamua kiuchumi bila ya kupata mafunzo yatakayowawezesha kuziona fursa zilizowazunguka na kuzitumia…nawaombeni elimu hii muitilie maanani,” alisema.
Dk. Lunyungu alisema kuwa Mkoa wa Iringa umezungukwa na aina mbalimbali ya vyakula na malighafi hivyo ni jukumu la kila mwananchi kutumia fursa zilizoko kujikomboa kiuchumi na kuleta maendeleo ya nchi.
Alifafanua kuwa mara baada ya washiriki hao kumaliza mafunzo, taasisi hiyo itawasaidia kuunda vikundi na uongozi wake lengo likiwa kufanya tathmini ya namna wajasirimalia hao watakavyotekeleza kwa vitendo mafunzo hayo.
Dk. Lunyungu alisema katika mafunzo hayo wajasiriamali wamefahamu kupamba, kutengeneza egg chop, karanga za mayai, clips, sambusa, mafuta ya mgando, mishumaa nguo za  batiki na vikoi.
Aliongeza pia kuwa wajasiriamali hao wamepata mafunzo ya ufugaji kuku, nyuki, kilimo cha Uyoga na usindikaji wa maziwa.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Powered by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Iringa Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa