Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
JESHI la Polisi Kitengo cha Usalama Barabarani Mkoa wa Iringa
limeweka mikakati ya kupunguza ajali za barabarani zinazozidi
kuongezeka kutokana na uzembe wa madereva wachache mkoani hapa.
Akizungumza na Tanzania Daima ofisini kwake jana, Mkuu wa Usalama
Barabarani, Kamanda Leopord Fungu, alisema ajali za barabarani limezidi
kuongezeka na kuwataka madereva kuwa makini na kufuata sheria za
barabarani bila shuruti.
Fungu alisema hatakuwa na mzaha kwa madereva wazembe hasa wanaotumia
barabara kuu ya Iringa kwenda mikoani na wakibainika adhabu kali
itachukuliwa dhidi yao ikiwemo faini pamoja na kifungo.
Chaanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment