Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Msafara wa Katibu Mkuu CCM Taifa Ukielekea Kata ya Nzihi kwaajili ya Kufunga Kampeni za Ubunge Jimbo la Kalenga-CCM.
Katika
Siku zote za Kampeni akina Baba na Akina-mama Wamekuwa Wakijitokeza
Barabarani kwaajili ya Kuishangilia CCM na Kuonesha Ishara ya Dole
kwamba Mambo Safi kwa Chama Cha Mapinduzi.
Mambo ya CCM Kalenga hayo.
CCM ipo mioyoni Mwetu
Ilikuwa
ni Kila Mtu anakimbilia Barabarani Kuishangilia CCM.Bibi ambaye Jina
halikufahamika akiwa na
Wajukuu Zake wakishangilia CCM.
Wajukuu Zake wakishangilia CCM.
CCM Kwa Raha Zetu
CCM hakuna Kulala Kalenga.
Wananchi wa Kalenga wakionesha Ishara ya Dole Gumba kwamba CCM Yatosha.
Watoto Pia Wanasema CCM Yatosha,Hapa wamesikia CCM wanapita Wakakimbilia Barabarani.
Ni CCM tu Kwa Walakalenga,Ilani ya Chama Cha Mapinduzi imetekelezwa Vizuri hapa Kalenga./
Katibu
Mkuu CCM-Mh.Kinana akizungumza na Kijana Wa Kata ya Nzihi hii leo
wakati anaelekea Kufunga Kampeni za Ubunge Jimbo la Kalenga.
Katika
Vijiji Vyote 89 ndani ya Jimbo la Kalenga,Mapokezi ya Mgombea wa Chama
Cha mapinduzi yalikuwa hivi.Hii Picha ni leo wakati wa Kufunga
Kampeni,Lakini Kuanzia Kufungua hadi Kufunga Wanakalenga Wamekuwa na
Mapenzi ya dhati kwa Kijana Wao na Wamejitokeza kwa Wingi sana kwenye
Mikutano yote Vijijini.
Uchaguzi wa Jimbo la Kalenga Unafanyika Tar.16/03/2014 na Vyama vilivyosimamisha Wagombea ni CCM,CHADEMA na CHAUSTA.
Katibu
Mkuu CCM,Naibu Katibu Mkuu CCM-Bara na Mgombea wa CCM Jimbo la Kalenga
wakiingia kwenye Uwanja wa
Mkutano Kata ya Nzihi Jimbo la Kalenga,Pia
walichukua muda kusalimiana na Wananchi wa Kata ya Nzihi waliokuwa na
Shauku ya Kusikia maneno ya Viongozi hawa wa Chama Cha Mapinduzi.Mapokezi Mazito ya Mgombea wa CCM Ndugu Godfrey William Mgimwa wakati wa Kufunga Kampeni hapa Kalenga hii leo.Katibu
Mkuu CCM akifurahia Jambo na Naibu katibu Mkuu-CCM Bara Mh.Mwigulu
Nchemba na Mgombea wa CCM Jimbo la Kalenga Ndugu Godfrey Mgimwa.Msanii
Dokii ambaye ni kada Mtiifu wa Chama Cha Mapinduzi akiimba wimbo
maalumu unaomuhusu Mgombea wa CCM Jimbo La Kalenga Ndugu Godfrey William
Mgimwa na anavyotakiwa Kutatua changamoto za Wanakalenga na Kutekeleza
Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kama alivyokuwa Mbunge wa CCM aliyefariki.Chifu
Mkwawa akizungumza na Wananchi wa kata ya Nzihi,Kubwa amewaomba
Kumpigia Kura Godfrey William Mgimwa Kwa sababu yeye Kama Chifu amekuwa
bega kwa bega na Chama Cha Mapinduzi na ameshuhudia Maendeleo Makubwa
yakifanywa na CCM hususani Ujenzi wa Hostel za Wasichana
Mashuleni,Umeme,Vituo vya AFya na Barabara zinazopitika wakati wote.Mh.Kangi Lugola
akiwaomba Wanakalenga Kumchagua Godfrey WIlliam Mgimwa hapo Kesho
kwasababu ni Kijana na ananidhamu,Amesema hahitaji kuona Wananchi
wanapoteza Muda kuchagua watu wanamtusi Rais wa Nchi,Wanatoka Bungeni
wakati wa Bajeti na Wamegeuza chama cha Ukoo.Katibu wa UVCCM Taifa Ndugu Sixstus Mapunda akiwahakikishia Wanakalenga Usalama wao katiaka Zoezi Zima la Kupiga Kura.Katibu
wa CCM Mkoa Wa Mtwara Ndugu.Akwilombe akitoa wito kwa Wanakalenga
kuacha kusikiliza Propaganda eti Godfrey William Mgimwa anarithi
Ubunge.Amewambia Godfrey amepatiakana katika Mchakato halali wa Kura za
Maoni tena ukihusisha wagombea 9.Wale wanaosema Kuwa Mgimwa anarithi
Ubunge ni Waongo kwa sababu wao Wenyewe Chama Kizima ni Mtu na Mdogo Mtu
au Mkwe na Mkwe au Baba na Mtoto(ameorodhesha U-familia ndani ya
Chadema).
Naibu
katibu Mkuu CCM-Bara Mh.Mwigulu Nchemba akisalimiana na Wananchi wa
Kata ya Nzihi hii leo wakati wa Kufunga Kampeni za Ubunge Jimbo la
Kalenga.
Naibu
Katibu Mkuu CCM Bara Mh.Mwigulu
Nchemba amewasihi Wanakalenga(kata ya Nzihi)Kuendeleza Wembe wa
Kuikataa CHADEMA kabisa kabisa katika Nchi hii kwasababu wamekuwa Vinara
wa Kusababisha Mauaji na Machafuko ya Amani katika Miji yetu.Pia
amesisitiza kuwa Uchaguzi huu Mdogo haubadirishi Serikali,Kwasababu
wenye Ilani ni CCM na Ilani Inayotekelezwa Kalenga niya CCM,Ametolea
Mfano kuwa Itawekazana Vipi Amefariki Muumini wa Kiislamu eti Unamwita
Askofu akaendeshe Mazishi,au Amefariki Mkristo unamuita Shekhe
akaendeshe Misa ya Mazishi??.Ni jambo lisilowezekana hata kidogo,CCM
ndio wenye Ilani Inayotekelezwa hivyo Mbunge anayetakiwa kusimamia Ilani
hiyo ni Godfrey William Mgimwa wa Chama Cha Mapinduzi.
Katibu Mkuu CCM Taifa Kanali Mstaafu Kinana akifunga rasmi Kampeni za Ubunge Jimbo la Kalenga kwa Chama Cha Mapinduzi,amewaomba sana Wanakalenga keuendelea Kuwa na Imani na Chama Cha Mapinduzi na Kesho Wananchi wajitokeze wakapige Kura kumchagua Godfrey William Mgimwa iliaendelee kutekeleza pale alipaochia Mbunge aliyefariki.
Katibu Mkuu CCM Taifa Kanali Mstaafu Kinana akifunga rasmi Kampeni za Ubunge Jimbo la Kalenga kwa Chama Cha Mapinduzi,amewaomba sana Wanakalenga keuendelea Kuwa na Imani na Chama Cha Mapinduzi na Kesho Wananchi wajitokeze wakapige Kura kumchagua Godfrey William Mgimwa iliaendelee kutekeleza pale alipaochia Mbunge aliyefariki.
Picha na Maelezo na Sanga Festo wa Habari Kwanza Media/Blog
0 comments:
Post a Comment