Diwani Elia Mgwila aliyesimama |
Mpiga kura akigonga mlango wa diwani bila mafanikio |
Nyumba ya aliyofumaniwa diwani huyo na mke wa mtu hii hapa
Hapa ni nyumbani kwa mheshimiwa mlango ukiwa umefungwa huku ufunguo ukiwa nje |
Mwananchi akitoka kumwona diwani huyo bila mafanikio leo
Kama ni kituko cha mwaka basi hiki pia ni kituko cha aina yake pamoja na diwani wa kata ya Ifunda jimbo la Kalenga wilaya ya Iringa mkoani Iringa Mheshimiwa Elia Mgwila kufumaniwa na kukatwa sikio moja na kung'olewa meno ila bado diwani huyo ambae ni majeruhi ameendelea kugoma katukatu kwenda Hospital kutibiwa majeraha hayo.
Wakizungumza na mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com kwa nyakati tofauti ndugu wa karibu wa diwani huyo mpenda vya watu wamesema kuwa mbali ya madiwani wenzake na viongozi wa CCM kumshawishi kwenda kutibiwa ila amegoma katakata kuwasikiliza .
Mbali ya kuwagomea ngudu na marafiki hao bado diwani huyo amegoma kwenda kituo cha polisi kufungua shitaka hilo na kudai kuwa yote anamwachia mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi na vyote vilivyopo duniani .
Wakati diwani huyo akigoma kufika Hospital kutibiwa taarifa zinadai kuwa jeshi la polisi ambalo lilikuwa likimshikilia bwana mwenye mke aliyefumaniwa na diwani huyo mkazi wa kijiji cha Ifunda kibaoni pamoja na mdogo wake na mkewe wameachiwa huru na jeshi la polisi ambalo lilikuwa likiwashikilia kwa tukio hilo la kumjeruhi diwani .
Huku habari za kipolisi zikidai kuwa watuhumiwa hao wameachiwa huru kutokana na diwani huyo kugoma kufungua kesi juu ya shambulio hilo la mwili.
Kwa Hisani ya Francis Godwin
0 comments:
Post a Comment